Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Yoane 2:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Wapenzi, siwaandikii amri mupya, lakini ile ya zamani muliyoijua tangia mbele. Na amri hiyo ya zamani ni lile neno mulilosikia.

Gade chapit la Kopi




1 Yoane 2:7
22 Referans Kwoze  

Usijilipize kisasi au kuwa na kinyongo juu ya wazao wa watu wako lakini umupende mwenzako kama vile unavyojipenda wewe mwenyewe. Mimi ni Yawe.


Kwa maana huu ndio ujumbe muliosikia tangia mbele: tupendane sisi kwa sisi.


Amri yake ndiyo hii tuamini jina la Mwana wake Yesu Kristo na tupendane sisi kwa sisi kama vile Kristo alivyotuamuru.


Mumupende Yawe, Mungu wenu, kwa moyo wenu wote, kwa roho yenu yote na kwa nguvu yenu yote.


Huyo mugeni anayekaa nawe atakuwa kwako kama vile mwenyeji nawe utamupenda kama vile unavyojipenda mwenyewe, kwa sababu nawe ulikuwa mugeni katika inchi ya Misri. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.


Kwa hiyo muchunge ndani ya mioyo yenu mafundisho muliyosikia tangia mbele. Kama mukichunga mafundisho yale muliyosikia tangia mbele, mutakaa ndani ya Mwana pamoja na Baba.


“Mumesikia kwamba imesemwa hivi: ‘Umupende mwenzako, lakini umuchukie adui yako.’


Halafu wakamukamata Paulo, na kumupeleka mbele ya Baraza Kubwa inayoitwa “Areopago,” wakamwuliza: “Unaweza kutujulisha maana ya mafundisho haya mapya unayotoa?


Ninawapa amri mupya: mupendane ninyi kwa ninyi. Kama mimi nilivyowapenda, nanyi mupendane vilevile.


Lakini wapendwa wangu, ijapokuwa tunasema hivi, hatuna mashaka juu yenu, tukijua kwamba munafuata njia nzuri zaidi, ile ya wokovu wenu.


Wapendwa wangu, sasa sisi ni watoto wa Mungu, wala namna tutakavyokuwa haijaonekana bado waziwazi. Lakini tunajua kwamba wakati Kristo atakapotokea, tutafanana naye kwa sababu tutamwona vile anavyokuwa.


Wapendwa wangu, zamiri yetu isipotuhukumu, sisi tuko na tumaini mbele ya Mungu.


Wapendwa wangu, musimwaminie kila mutu anayesema kwamba yuko na Roho wa Mungu, lakini mumupime kwa kuhakikisha kama roho yule anatoka kwa Mungu. Kwa maana manabii wengi wa uongo wametokea katika dunia.


Wapendwa wangu, tupendane, kwa maana upendo unatoka kwa Mungu. Kila mutu anayekuwa na upendo ni mutoto wa Mungu naye anamujua Mungu.


Wapendwa wangu, ikiwa Mungu alitupenda sisi namna ile, sisi vilevile tunapaswa kupendana.


Basi hii ndiyo amri tuliyopewa na Kristo: yule anayemupenda Mungu anapaswa kumupenda ndugu yake vilevile.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite