Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Yoane 2:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Sisi tunatambua kwamba tunamujua Mungu ikiwa tunashika amri zake.

Gade chapit la Kopi




1 Yoane 2:3
26 Referans Kwoze  

“Kama munanipenda, mutashika amri zangu.


Kama mukishika amri zangu, mutakaa katika upendo wangu, kama vile mimi nilivyoshika amri za Baba yangu na kukaa katika upendo wake.


Kwa maana kumupenda Mungu ni kutii amri zake. Na amri zake si ngumu,


“Sababu gani munaniita ‘Bwana, Bwana,’ nanyi hamufanyi yale ninayowaamuru?


Ninyi ni warafiki zangu, kama mukifanya sawa ninavyowaagiza.


Kwa njia hii tunatambua kwamba sisi tunakaa ndani ya Mungu, naye anakaa ndani yetu: yeye ametupatia Roho wake.


Na alipokwisha kufanywa kuwa mukamilifu, akawaongoza watu wote wanaomutii wapate kuokolewa kwa milele.


Nitafuatilia amri zako, maana unanifungua akili zaidi.


Kwa njia hii tutatambua kwamba sisi ni watu wa ukweli, na mioyo yetu itatulia mbele ya Mungu.


Nao uzima wa milele ni kukujua wewe unayekuwa peke yako Mungu wa kweli na Yesu Kristo uliyemutuma.


Tunajua kwamba sisi ni watoto wa Mungu ingawa dunia yote inatawaliwa na yule Mwovu.


Sisi tunajua kwamba tumeponyoka lufu na kupata uzima kwa sababu tunawapenda wandugu zetu. Mutu asiyekuwa na upendo ni kama mufu.


Yule Mungu aliyesema: “Mwangaza uangaze katika giza,” ndiye aliyeangaza ndani ya mioyo yetu, na kutuwezesha kufahamu utukufu wa Mungu unaongaa kwenye uso wa Kristo.


Heri wale wanaosafisha kanzu zao, kwa maana watakuwa na haki ya kukula matunda ya muti wa uzima na ya kuingia katika muji ule kwa kupitia kwenye milango.


Mungu anasema: Kisha kutaabika sana, mutumishi wangu atafurahi. Kwa njia ya kujulikana kwa huyo mutumishi wangu wa haki, atawafanya wengi wakuwe wenye haki, naye atazibeba zambi zao.


Nikichunguza amri zako zote, hapo kweli sitapata haya.


Ninawaandikia ninyi wababa, kwa sababu mumemujua yule aliyekuwa tangu mwanzo wa vitu vyote. Ninawaandikia ninyi vijana kwa sababu mumemushinda yule Mwovu.


Basi kila mutu anayeungana naye hafanyi tena zambi; lakini kila mutu anayefanya zambi hakumwona wala kumujua.


Wapendwa wangu, tupendane, kwa maana upendo unatoka kwa Mungu. Kila mutu anayekuwa na upendo ni mutoto wa Mungu naye anamujua Mungu.


Hii ndiyo namna tunavyojua kwamba tunawapenda watoto wa Mungu: kwa kumupenda Mungu na kushika amri zake.


Yule nyoka akamukasirikia yule mwanamuke na kwenda kufanya vita na wazao wake wengine; ndio wale wanaoshika amri za Mungu na kufuata ukweli ulioshuhudiwa na Yesu Kristo.


Kwa sababu hiyo, watu wa Mungu wanaoshika amri za Mungu na kumwamini Yesu wanapaswa kuwa wavumilivu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite