Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Yoane 2:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Watoto wangu wapendwa, ninawaandikia maneno hayo kusudi musitende zambi. Lakini kama mutu akitenda zambi, tuko na yule anayetutetea mbele ya Baba. Naye muteteaji yule ndiye Yesu Kristo, mwenye haki.

Gade chapit la Kopi




1 Yoane 2:1
47 Referans Kwoze  

Kwa maana kuna Mungu mumoja tu, na kuna mupatanishi mumoja tu kati ya Mungu na watu, ni yule mutu, Kristo Yesu,


Ni nani anayeweza basi kuwahukumu? Hakuna hata mumoja! Maana Yesu Kristo ndiye aliyekufa, na zaidi ya hiyo, alifufuka, na sasa anakaa na mamlaka kwa kuume kwa Mungu, na yeye ndiye anayetuombea.


Yesu akamujibu: “Mimi ni njia, ukweli na uzima. Mutu hawezi kufika kwa Baba asipopitia kwangu.


Kwa maana Kristo alikuwa bila zambi, lakini Mungu alimubebesha muzigo wa zambi zetu, kusudi kwa njia yake tupate kuwa wenye haki mbele ya Mungu.


Lakini ninyi, watoto wangu, muko watoto wa Mungu, nanyi mumewashinda manabii wa uongo; maana roho anayekaa ndani yenu ni mwenye uwezo kuliko yule anayekaa ndani ya watu wa dunia.


Watoto wangu, upendo wetu usikuwe wa masemi tu; lakini unapaswa kuwa upendo wa kweli na unaoonekana kwa matendo.


Watoto wangu, mutu asiwadanganye! Mutu anayetenda mambo ya haki ni mwenye haki kama vile Kristo ni mwenye haki.


Mwanamuke yule akamujibu: “Bwana, hakuna mutu.” Basi Yesu akamwambia: “Mimi vilevile sikuhukumu. Ujiendee, lakini usifanye zambi tena.”]


Kwa maana Kristo hakuingia katika Pahali Patakatifu palipojengwa na watu, panapokuwa tu mufano wa Pahali Patakatifu kamili, lakini aliingia katika mbingu yenyewe, pahali anaposimama sasa mbele ya Mungu kwa kututetea.


Ninyi munajua kwamba Yesu Kristo alikuja kusudi aondoe zambi, na hakuna zambi ndani yake.


Kwa maana, kwa njia ya Kristo sisi wote, Wayuda na watu wa mataifa mengine, tumefunguliwa njia ya kufika mbele ya Baba katika Roho mumoja.


Musitumikie chakula kinachoharibika, lakini mutumikie chakula kinachodumu na kuleta uzima wa milele. Mwana wa Mutu atawapa ninyi chakula hiki, kwa sababu Mungu Baba ametoa uhakikisho juu yake.”


Lakini, ukimwonya mutu wa haki asitende zambi, naye akiacha kutenda zambi, hakika mutu huyo ataishi, kwa sababu amepokea maonyo yako, nawe utakuwa umeyaokoa maisha yako.


Kufuatana na hiyo, Kristo naye alikufa mara moja tu kwa sababu ya zambi zenu. Yeye alikuwa mwenye haki kwa ajili ya waovu, kusudi awaonyeshe ninyi njia ya kumufuata Mungu. Aliuawa kimwili, lakini kwa uwezo wa Roho Mutakatifu alipata tena uzima.


Kama mukikasirika, musianguke katika zambi, kasirani yenu isidumu muchana kutwa,


Watoto wangu wapendwa, kama vile mwanamuke anavyopata uchungu wa kuzaa, mimi vilevile, ninapata tena uchungu kwa ajili yenu mpaka mutakapokuwa na hali inayokuwa kama ya Kristo ndani yenu.


kama vile Baba anavyonijua mimi, na mimi ninavyomujua Baba. Vilevile mimi ninatoa maisha yangu kwa ajili ya kondoo wangu.


Lakini mimi nina ushuhuda mukubwa zaidi kuliko ule uliotolewa na Yoane. Maana sasa mambo ninayofanya ndiyo Baba aliyoniamuru kutimiza, nayo yananishuhudia na kuonyesha kwamba yeye amenituma.


“Baba yangu, umeweka vitu vyote katika mikono yangu. Hakuna mutu anayemujua Mwana isipokuwa Baba, wala hakuna anayemujua Baba isipokuwa Mwana na yeyote ambaye Mwana anataka kumujulisha kwake.”


Yeye hakutenda zambi, wala neno la udanganyifu halikutoka ndani ya kinywa chake.


Mugeuze mafikiri, murudie katika usawa, muache kufanya zambi. Ninasema neno hili kwa kuwapatisha haya, kwa sababu wamoja kati yenu hawamujui Mungu.


Kisha Yesu akamukuta mutu yule ndani ya hekalu, akamwambia: “Angalia, sasa umepona. Basi usifanye zambi tena, kusudi jambo baya zaidi lisikufikie.”


Mushangilie sana enyi watu wa Sayuni! Mupige vigelegele, enyi watu wa Yerusalema! Angalia, mufalme wenu anawakujia, anakuja kwa shangwe na ushindi! Ni mupole, amepanda juu ya punda, juu ya mwana-punda, mutoto wa punda.


Dini inayokuwa safi na bila kosa mbele ya Mungu Baba ndiyo hii: kushugulikia wayatima na wajane wanaoteswa, na kujilinda mwenyewe na uchafu wa dunia hii.


Mujue kwamba Yawe amejichagulia mutu wake wa haki. Yawe anasikia kila mara ninapomwomba.


Watoto wangu wapendwa, muepuke kuabudu sanamu za miungu.


Kwa njia ya ulimi tunamusifu Bwana anayekuwa Baba yetu, na kwa njia ile ile tunalaani watu walioumbwa kwa mufano wa Mungu.


Ni nini basi? Tufanye zambi kwa sababu sisi hatuishi chini ya Sheria, lakini chini ya uwongozi wa neema ya Mungu? Hapana hata kidogo!


Watoto wangu, ningali pamoja nanyi kwa muda mufupi tu. Mutanitafuta, lakini sawasawa nilivyowaambia Wayuda, ninawaambia ninyi vilevile kwamba hamuwezi kufika pahali ninapokwenda.


Ninakuandikia barua hii, ijapokuwa ninatumaini kuja kukuona kisha muda kidogo.


Basi Yesu akawauliza: “Watoto wangu, mumepata samaki?” Wakamujibu: “Hapana.”


Nami nitamwomba Baba awape musaidizi mwingine kwa kukaa nanyi milele;


Ni nani kati ya manabii ambaye babu zenu walikosa kumutesa? Waliwaua wale waliotabiri zamani habari za kuja kwa Mwenye Haki. Na sasa mumemutoa na kumwua.


Basi ikiwa kama tulipokuwa waadui za Mungu tulipatanishwa naye kwa njia ya kufa kwa Mwana wake, inaonyesha zaidi sana kwamba tukiwa tumepatanishwa naye, tutaokolewa kwa njia ya uzima wa Kristo.


Kila tendo lisilokuwa la haki ni zambi, lakini kuna zambi isiyoleta kifo.


Hakuna jambo linalonifurahisha kuliko lile la kusikia kwamba watoto wangu wanaishi katika ukweli.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite