Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Yoane 1:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Tukisema kwamba hatuna zambi, tunajidanganya sisi wenyewe, wala ukweli hauko ndani yetu.

Gade chapit la Kopi




1 Yoane 1:8
33 Referans Kwoze  

kwa maana wote wamefanya zambi na kukosa utukufu wa Mungu.


Sisi wote tunakosa kwa njia mbalimbali. Mutu asiyekosa katika masemi yake, huyo ni mutu mukamilifu, naye yuko na uwezo wa kutawala mwili wake wote.


Hakika, hakuna mutu wa haki katika dunia anayetenda vizuri siku zote bila kutenda zambi.


Sisi wote tumepotea kama kondoo, kila mumoja wetu ameelekea njia yake. Lakini Yawe alimubebesha azabu, ambayo sisi wenyewe tuliistahili.


Mutu akijidai kwamba anamujua Mungu, lakini hashiki amri zake, yeye ni mwongo, nao ukweli hauko ndani yake.


Tukisema kwamba hatukutenda zambi, tunamugeuza Mungu kuwa mwongo, na ukweli wa neno lake si ndani yetu.


Nani anayesubutu kusema: “Nimetakasa moyo wangu; mimi nimetakasika na zambi yangu?”


Mutu ni nini hata aweze kuwa na moyo safi? Yule aliyezaliwa na mwanamuke atapata kuwa mwenye haki?


Kama mutu akijizania kwamba yeye ni kitu, ijapokuwa yeye si kitu, anajidanganya yeye mwenyewe.


Hakuna hata mumoja anayekuja kukuomba; hakuna anayejishugulisha kukutafuta. Wewe unauficha uso wako mbali nasi, umetuacha tufungwe na maovu yetu.


Usinitie katika hukumu mimi mutumishi wako, maana hakuna yeyote anayekuwa mwenye haki mbele yako.


Kama mutu akizani kwamba yeye ni mutu wa dini naye hawezi kuzuiza ulimi wake, anajidanganya mwenyewe, nayo dini yake haina faida.


na magomvi yasiyokuwa na mwisho ya watu wenye akili iliyokwisha kupotoka hata wamesahau ukweli kabisa. Ndio wale wanaozani kwamba dini ni njia ya kupata utajiri.


Mutu anaweza basi namna gani kuwa mwenye haki mbele ya Mungu? Mwanadamu tu anaweza namna gani kujidai kuwa safi?


“Ikiwa watatenda zambi mbele yako, maana hakuna mutu asiyetenda zambi, nawe ukiwakasirikia na kuwaacha washindwe na adui, hata wapelekwe mateka mpaka katika inchi ya adui inayokuwa mbali au karibu,


Mutu yeyote asijidanganye mwenyewe. Kama mutu fulani kati yenu akijizania kuwa mwenye hekima ya kidunia, ajifanye kama mupumbafu kusudi apate kuwa na hekima ya kweli.


Nani anayeweza kutoa kitu kisafi kutoka kitu kichafu? Hakuna anayeweza.


“Ikiwa watatenda zambi mbele yako, maana hakuna mutu asiyetenda zambi, na ukiwakasirikia na kuwaacha washindwe na waadui, hata wapelekwe kuwa watumwa mpaka inchi ya mbali au ya karibu,


kwa sababu ukweli huu unakaa ndani yetu nao utakuwa pamoja nasi hata milele.


Tukisema kwamba tunashirikiana naye, lakini tunaishi katika giza, tunasema uongo, nayo matendo yetu si ya kweli.


Musijidanganye ninyi wenyewe kwa kusikiliza tu neno la Mungu, lakini mulitimize kwa matendo.


Lakini watu waovu na wadanganyifu wataendelea katika maovu, wakipotosha watu wengine na kujipotosha wenyewe.


Kweli ninajua kama ni hivi. Lakini mutu anaweza namna gani kuwa haki mbele ya Mungu?


Nilifurahi sana wakati wandugu wamoja walipofika na kunielezea juu ya ukweli unaokuwa ndani yako na kwamba unaishi katika ukweli.


Watalipwa mateso kwa sababu ya mateso waliyoleta. Wanafurahia kutimiza waziwazi tamaa zao mbaya za kimwili muchana kati. Kufika kwao katika karamu zenu kunaleta haya na chukizo kubwa wanapofurahia mambo yao ya udanganyifu.


wewe unasema: Mimi sina kosa; hakika hasira yake imegeuka mbali nami. Lakini mimi nitakuhukumu kwa sababu unasema kwamba haukutenda zambi.


Baba yenu ni Shetani, nanyi munataka kutimiza sawa vile huyo baba yenu anavyotamani. Yeye ni mwuaji siku zote, naye hajasimama katika ukweli, kwa sababu ndani yake hakuna ukweli. Wakati anaposema uongo, masemi yake yanatokana na tabia yake, kwa sababu yeye ni mwongo na baba ya uongo.


Ni sawa ilivyoandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Hakuna hata mutu mumoja mwenye haki!


Kama mutu akisema “Ninamupenda Mungu,” naye anamuchukia ndugu yake, yeye ni mwongo. Kwa maana yule asiyemupenda ndugu yake anayemwona, hawezi kumupenda Mungu asiyemwona.


Kama ukoma umemushika na umeenea mwili muzima, toka kwenye kichwa mpaka kwenye miguu kama vile kuhani atakavyoona,


Halafu akamwuliza: “Wameona nini katika nyumba yako?” Hezekia akamujibu: “Wameona yote yanayokuwa katika nyumba yangu. Hakuna kitu chochote katika akiba zangu ambacho sikuwaonyesha.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite