Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Yoane 1:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Tukisema kwamba tunashirikiana naye, lakini tunaishi katika giza, tunasema uongo, nayo matendo yetu si ya kweli.

Gade chapit la Kopi




1 Yoane 1:6
25 Referans Kwoze  

Kama mutu akisema “Ninamupenda Mungu,” naye anamuchukia ndugu yake, yeye ni mwongo. Kwa maana yule asiyemupenda ndugu yake anayemwona, hawezi kumupenda Mungu asiyemwona.


Mutu akijidai kwamba anamujua Mungu, lakini hashiki amri zake, yeye ni mwongo, nao ukweli hauko ndani yake.


Tukisema kwamba hatukutenda zambi, tunamugeuza Mungu kuwa mwongo, na ukweli wa neno lake si ndani yetu.


watu wanaoacha njia zenye kunyooka kwa kufuata njia za giza,


Yesu akawaambia watu tena: “Mimi ni mwangaza wa dunia. Yeye anayenifuata hatatembea katika giza hata kidogo, lakini atakuwa na mwangaza wa uzima.”


Yesu akawaambia: “Mwangaza ungali kati yenu kwa muda kidogo. Mutembee wakati mungali na mwangaza, kusudi giza lisiwafunike, kwa sababu anayetembea katika giza hajui pahali anapokwenda.


Wandugu zangu, ni faida gani kama mutu akisema kwamba yuko na imani lakini haionyeshi kwa njia ya matendo mazuri? Ile imani itaweza kumwokoa?


Mimi nimekuja katika dunia kama mwangaza, kusudi mutu yeyote anayeniamini asikae katika giza.


Lile tuliloona na kulisikia, ndilo tunalotangaza kwenu vilevile, kusudi mupate kushirikiana nasi. Na huu ushirika wetu ni ule tunaokuwa nao pamoja na Baba na Mwana wake Yesu Kristo.


Lakini kama mutu akitembea usiku, anajikwaa, kwa sababu hana mwangaza ndani yake.”


Lakini mutu anaweza kusema: “Wewe uko na imani, na mimi niko na matendo.” Mimi nitajibu: “Unionyeshe imani yako pasipo matendo, na mimi nitakuonyesha imani yangu kwa njia ya matendo yangu.”


“Lakini ninyi hamujui wala hamufahamu! Ninyi munatembea katika giza la upotovu! Misingi yote ya haki katika dunia imetikiswa!


Tukisema kwamba hatuna zambi, tunajidanganya sisi wenyewe, wala ukweli hauko ndani yetu.


itakuwa na faida gani, kama mumoja wenu anamwambia: “Mwende vizuri, mukaote moto na kushiba,” lakini hamusaidii na kitu chochote?


Siku ile ya hukumu itakapotimia, wengi wataniambia: ‘Bwana, Bwana, sisi hatukutangaza ujumbe wa Mungu? Nasi hatukufukuza pepo kwa jina lako na kufanya maajabu mengi kwa jina lako?’


Wanadanganywa na watu wenye uongo na wanafiki wenye zamiri iliyokufa, iliyoharibika kabisa kama vile imeteketezwa kwa moto.


Wewe hauwezi kushirikiana na waamuzi wapotovu, wanaotunga masharti za kutetea maovu.


Ninyi hamumujui, lakini mimi ninamujua. Kama ningesema kwamba simujui, ningekuwa mwongo kama ninyi. Lakini ninamujua na ninashika neno lake.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite