Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Yoane 1:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Na hii ndiyo habari tuliyoisikia kutoka kwa Yesu Kristo na kuitangaza kwenu: Mungu ni mwangaza, na ndani yake hamuna giza hata kidogo.

Gade chapit la Kopi




1 Yoane 1:5
19 Referans Kwoze  

Yesu akawaambia watu tena: “Mimi ni mwangaza wa dunia. Yeye anayenifuata hatatembea katika giza hata kidogo, lakini atakuwa na mwangaza wa uzima.”


Kila zawadi nzuri na kila zawadi kamilifu inatoka juu kwa Mungu Baba aliyeumba miangaza yote inayokuwa katika mbingu. Mungu hawezi kubadilika wala kugeuka.


Hautahitaji tena jua kukuangazia muchana, wala mwezi kukuangazia usiku; maana mimi Yawe ni mwangaza wako milele; mimi Mungu wako nitakuwa utukufu wako.


Zaburi ya Daudi. Yawe ni mwangaza wangu na wokovu wangu, ni nani nitakayemwogopa? Yawe ni mulinzi wa maisha yangu, sitamwogopa mutu yeyote.


Ule mwangaza wa kweli, unaomwangazia kila mutu, unakuja katika dunia.


Yeye alikuwa chemichemi ya uzima, na uzima huu ulikuwa mwangaza kwa watu.


Wakati nikingali katika dunia, mimi ni mwangaza wa dunia.”


Hakutakuwa usiku tena, wala hawatakuwa na lazima ya mwangaza wa taa wala jua, kwa sababu Bwana wetu na Mungu wetu mwenyewe atawaangazia, nao watatawala milele na milele.


Muji ule hauna lazima ya mwangaza wa jua, wala wa mwezi, kwa sababu utukufu wa Mungu unauangazia na Mwana-Kondoo ndiye taa yake.


Unawashibisha kwa utajiri wa nyumba yako; unawakunywesha katika muto wa wema wako.


Ni yeye tu asiyeweza kufa na anayekaa katika mwangaza ambao mutu hawezi kukaribia. Hakuna mutu aliyemwona wala hakuna mutu anayeweza kumwona. Ndiye mwenye heshima na uwezo wa milele! Amina.


Siku moja tu ndani ya hekalu lako, ni bora kuliko siku elfu pahali pengine; afazali kubakia kwa mulango wa nyumba yako, kuliko kuishi ndani ya nyumba ya waovu.


Kwa maana huu ndio ujumbe muliosikia tangia mbele: tupendane sisi kwa sisi.


Kwa maana haya ndiyo mafundisho niliyopokea kutoka kwa Bwana, nami niliyotoa kwenu: katika usiku ule Bwana Yesu alipotolewa, alitwaa mukate,


kwako giza si giza hata kidogo, na usiku unaangaa kama muchana; kwako giza na mwangaza ni sawa.


Sasa, enyi wazao wa Yakobo, mukuje, tutembee katika mwangaza wa Yawe.


Anafunua siri na mafumbo, anajua kinachokuwa katika giza, mwangaza unakaa kwake.


Huu ndio ushuhuda wa Yoane kwa makuhani na Walawi waliotumwa na Wayuda kutoka Yerusalema kumwuliza kwamba yeye ni nani.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite