Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Wakorinto 9:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Mimi sina haki ya kujisifu kwa sababu ninatangaza Habari Njema, kwa maana nimelazimishwa kuitangaza. Basi ole kwangu kama nisipotangaza Habari Njema.

Gade chapit la Kopi




1 Wakorinto 9:16
21 Referans Kwoze  

Kwa sababu ninapaswa kwanza kuwaendea watu wote: Wagriki na wasiokuwa Wagriki, wenye elimu na wasiokuwa na elimu.


Mumwambie Arkipo aangalie vizuri atimize kazi ile aliyopewa na Bwana.


Lakini ninaposema “Sitamutaja tena Yawe, wala sitasema tena kwa jina lake”, ndani yangu kunawaka kitu kama moto uliofungiwa ndani ya mifupa yangu. Ninajaribu sana kuuzuia humo, lakini ninashindwa.


Lakini Yesu akamujibu: “Mutu yeyote anayeanza kulima na kuanza tena kuangalia nyuma hafai kutumika katika Ufalme wa Mungu.”


Kwa maana sisi hatuwezi kuacha kusema juu ya mambo tuliyoyaona na kuyasikia.”


Simba akinguruma, ni nani asiyeogopa? Bwana wetu Yawe akisema, ni nani atakataa kuutangaza ujumbe wake?


Basi katika kuungana kwangu na Kristo, ninaweza kujisifu kwa ajili ya kazi hii ninayomutumikia Mungu.


Lakini Bwana akamwambia: “Kwenda tu, kwa maana nimemuchagua mutu huyu kwa kunitumikia, kusudi atangaze jina langu kwa mataifa, kwa wafalme na kwa Waisraeli.


Lakini simama, uingie katika muji, na mule watakuambia jambo unalopaswa kufanya.”


Ikiwa Abrahamu alihesabiwa haki mbele ya Mungu kwa njia ya matendo yake, angeweza kujivuna. Lakini hawezi kujivuna mbele ya Mungu.


Yawe alinitosha katika kazi yangu hiyo ya uchungaji, akaniamuru nikuje kuwaambia watu wake wa Israeli unabii.


Basi, mimi nikasema: Ole kwangu! Mimi nimeangamia, maana, midomo yangu ni michafu, na watu ninaoishi nao ni wenye midomo michafu. Hata hivyo, kwa macho yangu mwenyewe, nimemwona Mufalme, Yawe wa majeshi.


Ee Yawe, wewe umenidanganya, nami kweli nimedanganyika; wewe una nguvu kuliko mimi, nawe umeshinda. Nimekuwa mutu wa kuchekelewa kila siku, kila mutu ananizarau.


Sasa basi, wewe Yeremia ujiweke tayari. Simama! Uende kuwaambia mambo yote ninayokuamuru. Usiwaogope, kusudi mimi nisikufanye kuwa mwoga mbele yao.


Tena kwa upande wangu haitatokea niache kuwaombea kwa Yawe; kufanya hivyo itakuwa kumukosea Yawe. Nitaendelea kuwafundisha njia njema na ya haki.


Hivi kuelekea maisha yenu na Kristo, hata mukiwa na walezi maelfu muko tu na baba mumoja. Kwa maana kuelekea maisha yenu na Yesu Kristo ni mimi niliyewazaa kwa njia ya kuwatangazia Habari Njema.


Ikiwa wengine wako na haki ya kupata vitu kama vile toka kwenu, sisi hatuna haki zaidi kuliko wao? Sisi hatudai kutendewa sawa na haki yetu, lakini tunavumilia kusudi tusiiwekee Habari Njema ya Kristo kizuizo chochote.


Vilevile, Bwana aliagiza kuwa wale wanaohubiri Habari Njema wanapaswa kuishi kwa njia ya Habari Njema.


Wakati nilipofika katika muji Troa kwa kutangaza Habari Njema ya Kristo, Bwana alinipatia wakati muzuri wa kutumika kule.


Mara moja yule mutumishi aliyepata furushi tano, akaenda kufanya uchuuzi na mali ile, akafaidia zingine tano.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite