Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Wakorinto 7:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Lakini kwa ajili ya kuepuka uasherati inafaa kila mwanaume akuwe na muke wake wa pekee, na kila mwanamuke akuwe na mume wake wa pekee.

Gade chapit la Kopi




1 Wakorinto 7:2
14 Referans Kwoze  

Hivi vilevile waume wanapaswa kupenda wake wao kama vile wanavyopenda miili yao wenyewe. Yule anayependa muke wake, anajipenda yeye mwenyewe.


Ingawa hivi, kwa ngambo yenu vilevile, kila mume anapaswa kumupenda muke wake kama vile anavyojipenda, na kila muke anapaswa kuheshimu mume wake.


Lakini kama hawawezi kujizuiza wao wenyewe, basi waoane; kwa maana afazali kuoa kuliko kuwaka tamaa.


Anayemupata muke amepata kizuri; ni zawadi kutoka kwa Yawe.


Muepuke uzinzi! Zambi ingine yoyote mutu anayofanya haigusi mwili wake, lakini yule anayefanya uzinzi anafanya zambi juu ya mwili wake mwenyewe.


Wao wanafundisha kwamba ni vibaya kuoana, na wanawakataza watu kula vyakula fulani fulani. Lakini Mungu aliumba vyakula vile kusudi watu waliokwisha kumwamini na kutambua ukweli wapate kuvitumia wakisha kumushukuru.


Munauliza: Mbona sasa hazikubali? Yawe hazikubali kwa sababu anajua wazi kwamba umeivunja ahadi yako kwa muke wa ujana wako. Umekosa uaminifu kwake ingawa uliahidi mbele ya Mungu kwamba ungekuwa mwaminifu kwake.


Nyumba na mali ni urizi mutu anaopata kwa babu zake, lakini muke mwenye akili anatoka kwa Yawe.


Lakini mimi ninawaambia: mutu yeyote anayeachana na muke wake, isipokuwa tu kwa sababu ya uzinzi, anamufanya muke yule kuwa muzinzi kama akiolewa tena. Na mutu anayemwoa yule muke aliyefukuzwa, anazini vilevile.


Sasa tuangalie mambo yale muliyoniandikia. Ni vizuri mwanaume asioe.


Mume anapaswa kumutimizia muke wake mapaswa yake, na muke anapaswa kumutimizia mume wake mapaswa yake.


Kila mwanaume anapaswa kujua namna ya kuishi na muke wake katika hali ya utakatifu na ya heshima,


Baba zao au kaka zao wakikuja kutulalamikia tutawaambia: “Sisi tunawaomba muwahurumie watu wa Benjamina na kuwaacha watwae hao wanawake; maana hatukupata wanawake wa kutosha katika vita ya Yabesi-Gileadi. Na kwa sababu si ninyi wenyewe muliowapatia hao wabinti zenu, hamutahukumiwa kwamba mumevunja kiapo.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite