Lakini niliwaandikia kwamba musishirikiane na mutu anayejiita ndugu mwamini, akiwa mwasherati, mwenye tamaa, mwenye kuabudu sanamu, mutukanaji, mulevi au munyanganyi. Na zaidi ya ile musichangie chakula na mutu wa namna hii.
chuki, uuaji, ulevi, ulafi, na mambo mengine yanayofanana na hayo. Ninawaonya tena kama vile nilivyowaonya mbele, kwamba watu wanaotenda mambo kama hayo hawatashiriki katika Ufalme wa Mungu.
Kuelekea maneno hayo, mutu yeyote asimukosee ndugu yake wala kumudanganya. Tumekwisha kuwaambia na kuwahakikishia mbele kwamba Bwana atawaazibu wale wanaofanya mambo kama hayo.
(Hakusema maneno haya kwa sababu aliwasikilia wamasikini huruma, lakini kwa sababu alikuwa mwizi. Ni yeye aliyekuwa akichunga mufuko wa feza, naye alikuwa akijitwalia mali toka ndani yake.)
“Ole kwenu, ninyi walimu wa Sheria na Wafarisayo, ninyi wanafiki! Munawafungia watu wengine njia ya kuingia katika Ufalme wa mbinguni. Ninyi wenyewe hamwingii mule na zaidi ya hii munawazuiza wale wanaotaka kuingia. [
Akaona muti wa tini pembeni ya njia, akaenda karibu nao, lakini hakuona kitu juu yake isipokuwa majani matupu. Halafu Yesu akaulaani muti ule akisema: “Wewe usitoe tena matunda tangu leo hata milele!” Na pale pale muti ule ukakauka.
Wakubwa wako ni waasi; wanashirikiana na wizi. Kila mumoja anapenda kituliro, na kukimbilia zawadi. Hawamupatii yatima haki yake, haki za wajane si kitu kwao.
Munazani kwamba hekalu hili linalojulikana kwa jina langu limekuwa kimbilio la wanyanganyi? Mujue kwamba mimi nimeona yote munayofanya! –Ni ujumbe wa Yawe.–
“Basi sasa ninawaweka chini ya ulinzi wa Mungu na wa neno lake la neema linaloweza kuwajenga katika imani na kuwapa urizi pamoja na watu wake wote watakatifu.
Wandugu zangu, muangalie, jambo ninalotaka kusema ni hili: kile kilichoumbwa kwa nyama na damu hakiwezi kupata urizi katika Ufalme wa Mungu katika hali ile, wala hakuna chenye hali ya kuharibika kinachoweza kuwa na hali ya kutoharibika.
Mujue waziwazi kwamba mwasherati yeyote na muchafu na mwenye tamaa ya mali (mwenye tamaa ni kama mwenye kuabudu sanamu), hao wote hawatapewa sehemu ya urizi katika Ufalme wa Kristo na Mungu.