Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Wakorinto 5:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Hiyo sikusema kabisa kwamba musishirikiane na wote wanaokuwa wazinzi katika dunia hii, wala wenye tamaa, wala wanyanganyi, wala wenye kuabudu sanamu. Kwa maana kwa kujitenga nao, ingewapasa kutoka katika dunia!

Gade chapit la Kopi




1 Wakorinto 5:10
18 Referans Kwoze  

Kama mupagani anawaalika kula chakula, nanyi mukikubali kwenda kule, mukule vyote wanavyotoa kwenu bila kuulizauliza neno kwa sababu ya zamiri.


Basi yule nyoka mukubwa akafukuzwa. Yeye ndiye yule nyoka wa zamani anayeitwa “Mwovu” au “Shetani,” anayedanganya watu wote. Akatupwa katika dunia pamoja na wamalaika zake.


Tunajua kwamba sisi ni watoto wa Mungu ingawa dunia yote inatawaliwa na yule Mwovu.


Manabii wa uongo ni watu wa dunia, ndiyo maana wanasema mambo ya kidunia nao watu wa dunia wanawasikiliza.


kusudi mupate kuwa bila kosa na kuwa na maisha safi. Hivi mutakuwa watoto wakamilifu wa Mungu wasiokuwa na kilema kati ya watu waovu na wapotovu wa dunia hii. Munapaswa kuangaza kati ya watu hawa kama vile nyota zinavyoangaza katika mbingu,


Mulikuwa mukiishi kufuatana na mwenendo mubaya wa dunia hii. Mulitii mutawala wa roho zenye uwezo wa anga anayetawala sasa watu wasiomutii Mungu.


Wao hawaamini kwa sababu yule mungu wa dunia hii amefunika akili zao. Yeye anawazuiza wasione mwangaza unaoletwa na Habari Njema ya utukufu wa Kristo, anayefanana na Mungu.


Basi, tuseme nini juu ya wenye hekima, walimu wa Sheria, nao wafundi wa usemi siku hizi? Mungu ameonyesha wazi kwamba hekima ya dunia hii ni upumbafu!


Yesu akawajibu: “Ninyi munatoka hapa chini, lakini mimi nimetoka juu. Ninyi ni wa dunia hii, lakini mimi si wa dunia hii.


Wapendwa wangu, tupendane, kwa maana upendo unatoka kwa Mungu. Kila mutu anayekuwa na upendo ni mutoto wa Mungu naye anamujua Mungu.


“Ninawaombea wao; siwaombei watu wa dunia, lakini hao ulionipa, kwa sababu wao ni wako.


“Nimekujulisha kwa watu wale ulionipa, ukiwachagua katika dunia. Wao walikuwa watu wako, uliwatoa kwangu, nao walishika neno lako.


Kama mungekuwa watu wa dunia, dunia ingewapenda, kwa maana ninyi ni watu wake. Lakini nimewachagua ninyi toka dunia hii, na ninyi si watu wa dunia tena. Ni kwa sababu hii dunia inawachukia.


Yule Mufarisayo akajitenga na mwenzake akiomba hivi: ‘Ee Mungu, ninakushukuru kwa sababu mimi si kama watu wote wengine wanaokuwa wanyanganyi, watenda maovu, wazinzi. Ninakushukuru vilevile kwa kuwa mimi si kama huyu mulipishaji wa kodi.


Katika barua niliyowatumia, niliwaandikia kwamba musishirikiane na washerati.


Lakini niliwaandikia kwamba musishirikiane na mutu anayejiita ndugu mwamini, akiwa mwasherati, mwenye tamaa, mwenye kuabudu sanamu, mutukanaji, mulevi au munyanganyi. Na zaidi ya ile musichangie chakula na mutu wa namna hii.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite