Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Wakorinto 4:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Sasa mumekwisha kupata vyote munavyohitaji! Mumekwisha kuwa watajiri! Munakuwa wafalme ingawa sisi hatuko wafalme. Heri mungekuwa kweli watawala kusudi nasi vilevile tupate kutawala pamoja nanyi.

Gade chapit la Kopi




1 Wakorinto 4:8
27 Referans Kwoze  

Umewapatia ufalme wa kikuhani kusudi wamutumikie Mungu wetu; nao watatawala katika dunia.”


Kama mutu akijizania kwamba yeye ni kitu, ijapokuwa yeye si kitu, anajidanganya yeye mwenyewe.


Tunafurahi wakati ninyi munapokuwa na nguvu, hata ikiwa sisi ni zaifu. Nasi tunawaombea kusudi mupate kuwa wakamilifu.


Hamuna kitu cha kujivunia! Hamujui vizuri mufano unaosema kwamba chachu kidogo inachachisha donge zima?


Kwa maana katika kuungana kwenu na Kristo, mumejaliwa katika vitu vyote, zaidi sana katika mambo yanayoelekea masemi na ufahamu.


Kufuatana na neema niliyopewa na Mungu, ninawaambia ninyi wote: mutu asijiwazie kuwa na ukubwa kupita vile inavyomustahili. Lakini mukuwe na mawazo ya ukadirifu, kila mumoja kulingana na kipimo cha imani aliyopewa na Mungu.


Ole kwenu ninyi munaoshiba sasa, maana mutasikia njaa. Ole kwenu ninyi munaocheka sasa, maana mutahuzunika na kulia.


Kuna mutu anayejidai kuwa tajiri, kumbe hana kitu. Mwengine anajiona kuwa masikini wakati ana mali tele.


Wewe unajidai kwamba uko tajiri mwenye mali mengi, wala haukosewi kitu. Lakini haujui kwamba wewe ni mukosefu, mwenye taabu, masikini, kipofu na mwenye kuwa uchi.


Basi wapendwa wangu, mulionyesha utii wenu siku zote wakati nilipokuwa kwenu, na sasa ingekuwa vema muendelee kufanya vile katika siku hizi ninapokuwa mbali nanyi. Mutumike kwa ajili ya wokovu wenu kwa woga na kutetemeka,


Kitu cha lazima ni kwamba mukuwe na mwenendo unaolingana na mafundisho ya Habari Njema ya Kristo. Kwa hivi hata kama nikikuja kuwaona au hata kama nisipokuja, nipate tu kusikia kwamba munasimama imara katika nia moja, na kwamba wote pamoja munapigana vita kwa ajili ya imani inayotokana na Habari Njema.


Ingekuwa heri muvumilie kidogo masemi yangu ya upumbafu! Ninawaomba kweli munivumilie!


Watu wamoja kati yenu wanajivuna wakifikiri kwamba sitakuja kuwaona.


Paulo akajibu: “Ikiwa wakati kidogo au wakati murefu, ninamwomba Mungu, si juu yako wewe mwenyewe tu, lakini hata hawa wote wanaonisikiliza leo wapate kuwa sawa mimi, lakini wasifikie tu kutiwa katika kifungo!”


Ikuwe hivyo! Yawe afanye hivyo. Yawe ayatimize maneno uliyotabiri, avirudishe hapa vyombo vya nyumba ya Yawe kutoka Babeli pamoja na watu wote waliohamishiwa huko.


Ole kwao wanaojiona kuwa wenye hekima na akili.


Kama vile mawingu na upepo bila mvua, ndivyo anavyokuwa mutu anayeahidi zawadi na haitoi.


Lakini Musa akamujibu: Unaona wivu kwa ajili yangu? Heri Yawe angewapa watu wake wote roho yake nao wapate kuwa manabii!


Yesu alipoona yale makundi ya watu, alipanda kwenye kilima. Alipokwisha kuikaa, wanafunzi wake wakamujongelea.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite