Kwa wakati huu ninapokuwa mbali nanyi, ninarudilia kuwaambia waziwazi maneno yale niliyokuwa nimekwisha kuwaambia mbele katika safari yangu ya pili niliyofanya kwenu. Ninawaambia kwamba nitakapokuja kwenu mara tena, sitakosa kuazibu wale waliofanya zambi zamani na wengine wote.
ijapokuwa sisi ni mitume wa Kristo, tungeweza kudai mambo fulani kwenu. Lakini sisi tulionyesha upole kati yenu kama vile mama anavyosumbuka kwa ajili ya watoto wake.
Ni kwa hiyo ninawaandikia maneno haya nikiwa mbali nanyi, kusudi wakati nitakapokuwa kati yenu nisitende kwa ukali kadiri ya mamlaka Bwana aliyonipa. Kwa maana uwezo ule ni kwa ajili ya kuwajenga katika imani, lakini si wa kubomoa.
Ni kwa sababu hii niliwaandikia kwamba sitakuja tena kwenu nisihuzunishwe na watu waliopaswa kunifurahisha. Maana nina uhakika kwamba mimi ninapofurahi, ninyi wote munafurahi vilevile.
Lakini hekima inayotoka mbinguni, kwanza ni safi, tena ni yenye amani, upole na usikilivu, inajaa huruma na matendo mema. Haina upendeleo wala udanganyifu.
Kwa maana sioni haya hata kama nimejivuna zaidi kwa ajili ya uwezo Bwana aliotupatia sisi. Kwa maana uwezo ule ni kwa ajili ya kuwajenga katika imani, lakini si wa kubomoa.
Nilimusihi Tito aende kwenu na nimemutuma pamoja na ndugu mwingine. Munaweza kusema kwamba Tito amewaibia ninyi? Basi mimi pamoja naye tuliishi katika nia moja na kuwa na mwenendo mumoja.
Wandugu zangu, kama mutu akipatikana na kosa fulani, ninyi munaoongozwa na Roho wa Mungu mumwonye mutu yule kwa roho ya upole. Na kila mumoja wenu ajiangalie mwenyewe, kusudi asijaribiwe vilevile.