Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Wakorinto 4:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Lakini nitakuja kwenu upesi Bwana akitaka. Basi pale nitajua maneno ya wale wanaojivuna na kujionea uwezo wao vilevile!

Gade chapit la Kopi




1 Wakorinto 4:19
18 Referans Kwoze  

Alipoagana nao, akawaambia: “Kama Mungu akitaka nitarudi huku kwenu tena.” Halafu akaondoka Efeso, akisafiri kwa njia ya chombo.


Nyuma ya mambo yale, Paulo alikusudia kwenda Yerusalema, akipitia katika inchi ya Makedonia na katika jimbo la Akaya. Akasema: “Nikisha kufika kule, ni lazima niende Roma vilevile.”


Ninamutaja Mungu kuwa mushuhuda wangu, yeye anajua roho yangu! Mimi nilikusudia kutorudia tena Korinto kwa sababu ya kuwasikilia huruma.


Kama mutu akiwa na njaa, akule katika nyumba yake, kusudi musikusanyike kwa kujiletea azabu. Basi maneno mengine yanayobaki nitayatengeneza wakati nitakapofika kwenu.


Watu wamoja kati yenu wanajivuna wakifikiri kwamba sitakuja kuwaona.


Ingawa vile, mimi ninatangaza mambo ya hekima kwa watu waliokomaa kiroho. Lakini mambo haya si ya hekima ya kidunia, wala ya watawala wa dunia hii watakaoangamizwa.


Na hivi Mungu akitaka, nitakuja kwenu kwa furaha, nami nitapata kutulizwa moyo kati yenu.


Ninyi mungepaswa kusema: “Kama Bwana anataka, tutaishi na kufanya hivi na hivi.”


Nitakuja kwenu kisha kupitia Makedonia kufuatana na mupango wangu wa kupitia kule.


Ninataka ninyi wote museme kwa luga za ajabu, lakini ninataka zaidi tena mupate kutabiri. Kwa maana, yule anayetabiri ni wa lazima kuliko yule anayesema kwa luga za ajabu, isipokuwa kama huyo mutu anaweza kutafsiri yale anayosema kusudi kanisa zima lijengwe katika imani.


Alipita katika inchi ile akiwaambia wanafunzi maneno mengi ya kuwatia moyo. Kisha akaenda Ugriki,


Wandugu zangu, nimesema maneno haya nikitwaa mufano wa Apolo na wangu mimi mwenyewe kusudi yakuwe fundisho kwenu. Nilitaka kwamba kufuatana na mufano huu mujifunze maana ya masemi haya: “Musipite pembeni ya maandiko.” Hata mutu mumoja kati yenu asijivunie mutu fulani na kuzarau mwingine.


Kwa maana sitaki kuonana nanyi kwa kupita tu. Ninatumaini kukaa pamoja nanyi siku chache Bwana akitaka.


Sitaki kuonekana kwamba ninataka kuwaogopesha kwa barua zangu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite