Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Wakorinto 16:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Sasa juu ya muchango unaofanyika kwa ajili ya watu watakatifu wa Mungu wanaokuwa Yerusalema; ninyi vilevile mufanye sawa vile nilivyoagiza makanisa ya Galatia.

Gade chapit la Kopi




1 Wakorinto 16:1
20 Referans Kwoze  

Mutu akiwa na mali ya dunia hii naye akimwona ndugu yake katika hitaji, lakini hataki kumusikilia huruma, mutu yule anaweza kusema kwamba anamupenda Mungu?


Muwasaidie watu wa Mungu katika mahitaji yao na muwakaribishe wageni.


Lakini kitu kimoja walichotuomba ni kukumbuka wamasikini wa makanisa yao, nami nimefanya vile kwa bidii.


“Nyuma ya kupitisha miaka mingi mbali na muji, nilirudi kule Yerusalema kuwaletea watu wa taifa langu musaada wa mali na kumutolea Mungu sadaka.


Ndugu, upendo wako umenifurahisha sana na kunifariji, kwa maana umetuliza mioyo ya watu wa Mungu.


Kwa maana ninasikia namna unavyomwamini Bwana Yesu na namna unavyowapenda watu wote wa Mungu.


Kwa maana Mungu ni mwenye haki. Yeye hatasahau kazi yenu na upendo mulioonyesha kwa ajili yake kwa namna mulivyowasaidia watu wake na munavyoendelea kuwasaidia.


Nao wakafanya vile, wakatuma misaada waliyokusanya kwa wazee wa kanisa kwa mukono wa Barnaba na Saulo.


Paulo na wale waliomusindikiza wakapita katika inchi ya Furigia na ya Galatia kwa sababu Roho Mutakatifu alikuwa amewakataza wasihubiri Neno la Mungu katika jimbo la Azia.


Alipokwisha kukaa Antiokia kwa siku chache, akaondoka kule, akapita muji kwa muji toka katika inchi ya Galatia mpaka katika inchi ya Furigia, na kule akawatia wanafunzi nguvu.


Na mumoja wao, aliyeitwa Agabo, akasimama, akatabiri kwa njia ya Roho Mutakatifu kwamba kutakuwa njaa kubwa katika dunia nzima. (Nayo ikatokea katika nyakati za utawala wa mufalme Klaudio wa Roma.)


Petro akamushika mukono na kumusimamisha wima. Kisha akawaita wanafunzi na wajane, akamupeleka mbele yao akiwa muzima.


Anania akajibu: “Bwana, nimekwisha kusikia watu wengi wakisema habari za mutu huyo, wakieleza mabaya aliyowatendea watu wako watakatifu wanaokuwa Yerusalema.


Ni kwa sababu hii ninawatumia ninyi Timoteo. Yeye ni mwana wangu mupendwa na mwaminifu mbele ya Bwana. Atawakumbusha kanuni ninazofuata katika maisha yangu na Yesu Kristo, nami ninazofundisha fasi zote katika makanisa yote.


Kama mutu akiwa na njaa, akule katika nyumba yake, kusudi musikusanyike kwa kujiletea azabu. Basi maneno mengine yanayobaki nitayatengeneza wakati nitakapofika kwenu.


Ninyi munajua Stefana na jamaa yake; munafahamu kwamba walikuwa watu wa kwanza walioamini katika inchi ya Akaya, nao wamejitoa kwa kutumikia watu wa Mungu. Hivi ninawasihi sana wandugu zangu,


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite