Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Wakorinto 14:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Mujikaze mukuwe na upendo. Vilevile mutamani sana kupata zawadi za Roho, hasa zaidi zawadi ya kutabiri.

Gade chapit la Kopi




1 Wakorinto 14:1
29 Referans Kwoze  

Kwa hiyo wandugu zangu, mutamani sana kupata zawadi ya kutabiri, nanyi musiwazuize watu kusema kwa luga za ajabu.


Mujikaze kwa kuishi katika amani na watu wote na kuishi katika utakatifu, kwa sababu hakuna mutu asiyeishi katika hali hiyo atakayemwona Bwana.


Usiache kutumia ile zawadi ya kiroho inayokuwa ndani yako, uliyopokea kutokana na maneno ya manabii na kwa njia ya kuwekewa mikono na wazee wa kanisa.


Mutende mambo yenu yote katika upendo.


Sasa tuangalie mambo yanayoelekea zawadi za Roho Mutakatifu. Wandugu zangu, sitaki mukose kufahamu ukweli wa zawadi hizi.


Basi sasa, hivi vitu vitatu vinadumu: imani, tumaini na upendo; lakini kinachokuwa kikubwa kuliko hivi vingine ni upendo.


Musizarau ujumbe unaotoka kwa Mungu.


Mwenendo wa waovu ni chukizo kwa Yawe, lakini Mungu anawapenda wale wanaofuata mambo ya haki.


Lakini wewe mutu wa Mungu, uepuke mambo haya, ushikamane na haki, ibada, imani, upendo, uvumilivu na upole.


Kama mutu akizani kwamba yuko na zawadi ya unabii au zawadi ingine ya Roho, anapaswa kujua kwamba maneno haya ninayowaandikia ninyi ni amri ya Bwana.


Yawe anasema hivi: Munisikilize enyi munaotaka kukombolewa, ninyi munaonitafuta mimi Yawe. Muangalie jiwe mulilochongwa toka ndani yake, mulima mulimochimbuliwa.


Sherti ajulikane kwa matendo yake mema. Anapaswa kuwa mutu aliyeadibisha watoto wake vizuri, aliyekaribisha wageni, aliyewapokea watu wa Mungu akiwanawisha miguu, aliyewasaidia wenye taabu na aliyejitolea kwa kutenda mema ya kila namna.


Asifiwe Mungu, Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo! Yeye ndiye aliyetupatia baraka za kiroho za kila namna kutoka katika eneo la mbingu kwa njia ya kuungana kwetu na Kristo.


Basi mutamani sana zawadi inayokuwa bora zaidi. Lakini sasa, nitawaonyesha njia nzuri sana kuliko zote.


Anayetafuta haki na wema atapata uzima, haki, na heshima.


Mupendwa wangu, usifuate mufano mubaya, lakini ufuate mufano muzuri. Mutu anayetenda mema ni mutoto wa Mungu; lakini anayetenda mabaya hashirikiani na Mungu.


undugu juu ya kushikamana na ibada, na upendo juu ya undugu wenu.


Tuko na zawadi mbalimbali kwa kadiri ya neema tuliyopewa na Mungu. Aliyepewa zawadi ya unabii, anapaswa kutabiri kwa kadiri ya imani yake.


Ujiepushe na tamaa za ujana, utafute kuishi katika haki, imani, upendo na amani pamoja na watu wote wanaomwabudu Bwana kwa moyo safi.


Basi tuseme nini? Watu wa mataifa mengine waliokosa kutafuta kuhesabiwa haki mbele ya Mungu wamehesabiwa haki mbele yake kwa njia ya imani.


Basi kwa hiyo tujikaze sana kufanya mambo yale yanayoleta amani na yanayotusaidia kujengana katika imani.


Kisha, utafika kule Gibeati-Elohimu, pahali ambapo pana kambi ya waaskari wa Wafilistini. Pale, utakapokuwa unakaribia muji, utakutana na kundi la manabii. Manabii hao watakuwa wanatoka kwenye nafasi ya kuabudia na wakipiga vinubi, matari, filimbi na zeze, na watakuwa wanatabiri.


Hata nikiwa na zawadi ya kutabiri, na uwezo wa kujua mafumbo yote na maarifa yote; hata nikiwa na imani kubwa inayoweza kuhamisha milima; lakini kama sina upendo, mimi ni kitu bure.


Kwa hiyo, zawadi ya kusema luga za ajabu ni kitambulisho kwa wasioamini, lakini si kwa waamini. Na zawadi ya kutabiri ni kitambulisho kwa waamini, lakini si kwa wasioamini.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite