Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Wakorinto 13:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Upendo haukosi kuwa na adabu, hautafuti faida yake mwenyewe, haukasiriki upesi, nao hauhesabii mutu ubaya.

Gade chapit la Kopi




1 Wakorinto 13:5
37 Referans Kwoze  

Mutu asitafute faida yake mwenyewe, lakini faida ya mwenzake.


Wandugu zangu wapendwa, mukumbuke neno hili: kila mutu anapaswa kuwa mwepesi kwa kusikia, lakini asikuwe mwepesi kwa kusema na kukasirika.


Watu wengine wote wanatafuta faida yao wenyewe, lakini hawashuguliki na Yesu Kristo.


Kwa kumaliza, wandugu zangu, muweke mafikiri yenu juu ya mambo yote yanayokuwa ya kweli, ya heshima, ya haki, safi, ya kupendeza, nayo mambo yote yanayostahili sifa na ya utu wema.


Wandugu, ninyi muliitwa na Mungu kusudi mukuwe watu huru. Basi musitumie uhuru huu kuwa ruhusa ya kutimiza tamaa za mwili, lakini musaidiane kwa upendo.


kusudi kusikuwe mabishano katikati ya viungo vya mwili, lakini vyote visaidiane sawasawa.


Ndiyo kusema, Mungu ndiye aliyekuwa akipatanisha watu wote na yeye mwenyewe kwa njia ya Kristo bila kuhesabu makosa yao. Yeye ametupatia ujumbe wa upatanisho.


Mufanye kama vile mimi: ninajikaza kwa kupendeza watu wote katika mambo yote, maana sitafuti faida yangu mimi mwenyewe, lakini faida ya watu wote, kusudi waokolewe.


Kwanza, ninasikia kwamba munapokusanyika kuna matengano katikati yenu, nami ninasadiki kwamba nusu ya maneno yale ni ya kweli.


Lakini mimi ninawaambia: mutu yeyote anayemukasirikia ndugu yake anapaswa kuhukumiwa. Naye anayemwambia ndugu yake: ‘Hauna akili wewe!’ anapaswa kupelekwa kwenye tribinali kubwa. Naye anayemwambia: ‘Uko mwenda-wazimu!’ anastahili kutupwa katika jehenamu.


Yule Mufarisayo aliyemwalika Yesu alipoona vile, akajisemesha: “Kama mutu huyu angekuwa kweli nabii, angetambua mwanamuke huyu anayemugusa ni wa namna gani. Angetambua kwamba yeye ni mwenye mwenendo mubaya.”


Yesu akawakazia macho kwa kasirani, akihuzunika kwa sababu ya ugumu wao. Akamwambia yule mutu: “Nyoosha mukono wako.” Akaunyoosha, nao ukakuwa muzima tena.


Munajua vizuri ninyi wenyewe namna munavyopaswa kuiga mufano wetu. Kwa maana sisi hatukukuwa wavivu wakati tulipoishi pamoja nanyi.


Mutu akiona kwamba hamutendei muchumba wake vizuri, naye akitawaliwa na tamaa kwamba wangepaswa kuoana, basi afanye sawa vile anavyotaka. Yeye hafanyi zambi, waoane tu.


Naye Yesu akijua mafikiri yao, akawauliza: “Sababu gani munawaza maneno hayo mabaya?


Watu watatesana, kila mutu na mwenzake; vijana watawazarau wazee, na watu wa ovyo ovyo watawazarau wenye heshima.


wakubwa wa Waamori walimwambia bwana wao, Hanuni: “Unazani kwamba Daudi kwa kukutumia watu wa kukufariji anamuheshimu baba yako? Daudi hakuwatuma watu hawa kwako kwa kuuchunguza na kuupeleleza muji halafu wauteke?”


Ni kwa hiyo ninavumilia mambo yote kwa ajili ya watu ambao Mungu alijichagulia kuwa wake, kusudi wao vilevile wapate kuokoka na kupata utukufu wa milele unaopatikana kwa njia ya Kristo Yesu.


Nami nilikuwa kama kondoo mupole anayepelekwa kuchinjwa; sikujua kwamba shauri walilofanya lilikuwa juu yangu. Wao walisema: Tuuharibu muti pamoja na matunda yake, tumwue apate kusahaulika katika dunia, jina lake lisikumbukwe tena.


Mwenye kuwaka hasira haraka anatenda kipumbafu, lakini mwenye akili ana uvumilivu.


Musikilize! Mimi ninajua mawazo yenu yote, na mipango yenu ya kunizarau.


Musa akakasirika sana, akamwambia Yawe: Usikubali sadaka za watu hawa. Mimi sijatwaa punda wa mutu yeyote, wala sijamuzuru mutu!


(Musa alikuwa mutu munyenyekevu kuliko watu wengine wote waliokuwa katika dunia.)


Nilipojitetea kwa mara ya kwanza hakuna hata mutu mumoja aliyenisaidia; wote waliniachilia. Mungu asiwahesabie makosa yao!


Musa akawajibu watu wa makabila ya Gadi na Rubeni: Munataka kubaki hapa wakati wandugu zenu Waisraeli wanakwenda kwa vita?


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite