Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Wakorinto 12:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Basi mutu mumoja anapewa na Roho uwezo wa kusema maneno ya hekima, na mwingine uwezo wa kusema maneno ya ufahamu na Roho yule yule.

Gade chapit la Kopi




1 Wakorinto 12:8
30 Referans Kwoze  

Maana Yawe anawapa watu hekima; katika kinywa chake kunatoka maarifa na ufahamu.


Ninyi munakuwa na kila kitu kwa uwingi: imani, usemi, ufahamu, kuwa na bidii ya kila namna na upendo munaokuwa nao kwetu. Kufuatana na hiyo mukuwe vilevile na uwingi katika kazi hii ya kuwa na moyo wa kutoa.


Kwa maana katika kuungana kwenu na Kristo, mumejaliwa katika vitu vyote, zaidi sana katika mambo yanayoelekea masemi na ufahamu.


Unifundishe kutimiza mapenzi yako, maana wewe ni Mungu wangu! Roho wako muzuri aniongoze katika njia sawa.


Lakini Mungu amewaunganisha na Yesu Kristo, naye amemufanya Kristo kuwa hekima yetu. Kwa njia ya Kristo tunahesabiwa haki mbele ya Mungu, tumekuwa watu watakatifu wa Mungu, na kukombolewa toka zambi zetu.


Ukawapa Roho wako mwema kuwashauria; ukawapa mana kuwa chakula chao, na maji ya kunywa kwa kutuliza kiu chao.


Upendo haukomi hata kidogo. Lakini kutabiri kunatoweka, zawadi ya kusema kwa luga za ajabu inatoweka, na maarifa yanapita.


Akawajibu: “Ninyi mumefunuliwa kujua siri ya Ufalme wa mbinguni, lakini kwao si vile.


Yawe anasema: Mimi ninafanya nanyi agano hili: Roho wangu anayekuwa juu yenu, maneno niliyoyaweka katika kinywa chenu, hayataondoka kwenu hata kidogo, wala kwa watoto na wajukuu wenu, tangu sasa na hata milele.


Bwana wetu Yawe amenifundisha jinsi ya kusema, kusudi niwatie moyo wale waliochoka. Kila asubui ananipa hamu ya kusikiliza mambo anayotaka kunifundisha.


Lakini ile roho inayokuwa ndani ya mutu, ile pumzi ya Mungu Mwenye Uwezo, ndiyo inayomwezesha mwanadamu kufahamu.


na kumujaza Roho wangu. Nimemupatia ufahamu na akili, maarifa na ufundi,


Hata nikiwa na zawadi ya kutabiri, na uwezo wa kujua mafumbo yote na maarifa yote; hata nikiwa na imani kubwa inayoweza kuhamisha milima; lakini kama sina upendo, mimi ni kitu bure.


Anabadilisha nyakati na wakati, anaondoa na kuwatawalisha wafalme. Anawapa hekima wenye hekima, anawaongezea wenye maarifa ufahamu.


Hivi wandugu, muwachague wanaume saba kati yenu wenye ushuhuda muzuri, wenye kujazwa na Roho Mutakatifu na wenye hekima, kusudi tuwaweke kwa kazi hii.


Wandugu zangu, kwa ngambo yangu ninajua hakika kwamba ninyi munajaa wema, nanyi munafahamu yote yanayofaa na munaweza kushauriana vizuri.


Hakuna mutu anayeweza kujua mawazo ya mutu mwingine isipokuwa tu roho ya mutu inayokuwa ndani yake. Vilevile, hakuna anayejua mawazo ya Mungu isipokuwa Roho wa Mungu tu.


Kama vile Maandiko Matakatifu yanavyosema: “Ni nani anayejua mawazo ya Bwana? Ni nani anayeweza kumushauria?” Lakini sisi tuko na mawazo yanayotoka kwa Kristo.


Basi wandugu zangu, nitawafalia nini kama nikikuja kwenu na kusema nanyi katika luga za ajabu? Sitawafalia kitu pasipo kuwaelezea maneno ya ufunuo, au ya elimu, pasipo kuwatabiria au kuwafundisha.


Wandugu zangu, niseme nini basi? Wakati munapokusanyika kwa ibada, mumoja anaweza kuimba wimbo, mwingine kufundisha, mwingine kutoa ufunuo, mwingine kusema kwa luga za ajabu na mwingine anaweza kutafsiri. Na hayo yote yanapaswa kufanyika katika nia ya kujenga kanisa katika imani.


Jambo ambalo tunajivunia ni hili: zamiri yetu inayotuhakikishia kwamba tumeishi katika dunia na zaidi kati yenu katika uaminifu na ukweli tulivyojaliwa na Mungu. Sisi hatukuongozwa na hekima ya kimutu lakini na neema ya Mungu.


Lakini Mungu ashukuriwe, maana yeye ndiye anayetupatia ushindi siku zote katika ushirika wetu pamoja na Kristo. Anatutumia sisi kwa kutambulisha Kristo pahali pote kama vile harufu nzuri ya marasi inavyosambaa popote.


Yule Mungu aliyesema: “Mwangaza uangaze katika giza,” ndiye aliyeangaza ndani ya mioyo yetu, na kutuwezesha kufahamu utukufu wa Mungu unaongaa kwenye uso wa Kristo.


Tunaonyesha kwamba sisi ni watumishi wa Mungu kwa njia ya usafi wa moyo wetu, ya ufahamu, ya uvumilivu, ya wema wetu, ya Roho Mutakatifu, ya upendo wetu wa kweli,


Inaonekana kuwa mimi si mutu anayeelewa kusema, lakini kwa ngambo ya elimu, mimi ninaielewa sana. Nasi tumeonyesha hayo yote kila wakati na katika mambo yote.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite