Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Wakorinto 12:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Kuna kazi za namna mbalimbali, lakini Mungu ni mumoja anayewezesha watu wote kuzitimiza.

Gade chapit la Kopi




1 Wakorinto 12:6
12 Referans Kwoze  

Ni yule yule Roho mumoja anayetenda mambo hayo yote, akimupa kila mumoja zawadi mbalimbali kama anavyopenda.


Hivi yule anayepanda na yule anayenyweshea maji, wote si kitu; Mungu ndiye anayekuwa wa lazima kwa maana ni yeye anayeotesha mbegu.


Lakini Yesu akawajibu: “Baba yangu anatumika wakati wote, nami ninatumika vilevile.”


Kwa hiyo hakuna tena tofauti kati ya watu wa mataifa mengine na Wayuda, wenye kutahiriwa na wasiotahiriwa, wageni, washenzi, watumwa na watu huru. Lakini Kristo ni yote naye yuko katika wote.


Mungu mumoja, Baba ya watu wote, anayekuwa juu ya wote, anayetumika kwa njia ya wote, na anayekaa ndani ya wote.


awakamilishe katika kila tendo jema kusudi mupate kutimiza mapenzi yake; yeye atimize ndani yetu yale yanayomupendeza, kwa njia ya Yesu Kristo. Yesu atukuzwe milele na milele. Amina.


Ni kwa sababu hiyo ninatumika na kupigana kwa uwezo ninaopewa na Kristo, unaoniwezesha kufanya kazi kwa nguvu.


kwa maana Mungu anafanya kazi ndani yenu na kuwapa moyo wa kutaka na kutimiza mambo yanayolingana na mupango wake mwema.


Na wakati vitu vyote vitakapokuwa vimewekwa chini ya mamlaka ya Mwana, halafu yeye mwenyewe atajiweka chini ya mamlaka ya Mungu aliyemupa mamlaka juu ya vitu vyote, kusudi Mungu apate kutawala juu ya vyote kabisa.


Sikia! Mungu anamufanyia mwanadamu haya yote, tena mara mbili, mara tatu.


Kuna utumishi wa namna mbalimbali, lakini ni Bwana mumoja ndiye wanayemutumikia.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite