Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Wakorinto 12:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Kwa sababu hii ninataka mufahamu kwamba hakuna mutu ambaye anaongozwa na Roho wa Mungu anayeweza kusema: “Yesu alaaniwe,” na hakuna mutu anayeweza kusema: “Yesu ni Bwana,” kama asipoongozwa na Roho Mutakatifu.

Gade chapit la Kopi




1 Wakorinto 12:3
19 Referans Kwoze  

Si kusema kwamba sisi wenyewe tuko na uwezo wa kujitungia jambo hili, lakini uwezo wetu unatoka kwa Mungu.


Kama ukiitikia kwa kinywa chako mwenyewe kwamba Yesu ni Bwana na kuamini katika moyo wako kwamba Mungu alimufufua, utaokolewa.


Munaniita ‘Mwalimu’ na ‘Bwana,’ na munasema kweli, maana ni vile ninavyokuwa.


Ingawa hivi, kwa ngambo yetu sisi tuko na Mungu mumoja peke yake tu, ndiye Baba aliyeumba vitu vyote, nasi tunaishi kwa nguvu yake. Vilevile kuko Bwana mumoja tu, ndiye Yesu Kristo. Kwa njia yake vitu vyote viliumbwa, nasi tunaishi kwa nguvu yake.


“Wakati Musaidizi nitakayewatumia toka kwa Baba atakapokuja, atanishuhudia mimi. Yeye ni Roho wa ukweli, naye anakuja toka kwa Baba.


Na Yesu akawaambia: “Basi namna gani Daudi, akiongozwa na Roho, aliweza kumwita ‘Bwana’, akisema:


Lakini Yesu akajibu: “Musimukataze, kwa maana hakuna mutu anayefanya miujiza kwa jina langu, ambaye anaweza nyuma kidogo kusema vibaya juu yangu.


Kama mutu hamupendi Bwana, alaaniwe! Bwana wetu, kuja!


maiti yake isiachwe juu ya muti usiku wote, lakini mutaizika siku hiyohiyo. Maana mutu aliyetundikwa amelaaniwa na Mungu nanyi hamutachafua inchi yenu muliyopewa na Yawe, Mungu wenu, ikuwe urizi wenu.


Hii inatokana na kuona jinsi munavyomukubali mutu yeyote anayekuja kwenu na kuwahubiri habari za Yesu mwingine asiyekuwa yule sisi tuliyemuhubiri. Na zaidi ya hii munakubali upesi kupokea roho ingine na ujumbe mwingine vinavyokuwa tofauti na Roho au Habari Njema muliyopokea toka kwetu.


Ingekuwa heri nilaaniwe na kutengwa na Kristo kwa ajili ya wandugu zangu wa damu,


Siku moja ya kumwabudu Bwana, nikashikwa na Roho wa Mungu, nikasikia sauti kubwa, inayolia kama baragumu,


Kristo alitukomboa toka laana ya Sheria, akijitwalia laana hiyo kwa ajili yetu. Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Mutu yeyote anayetundikwa juu ya muti amelaaniwa.”


Basi kama mimi ninayekuwa Bwana na Mwalimu wenu nimewanawisha miguu, ninyi vilevile munapaswa kunawishana miguu.


Yawe awalipe hayo hao watu wanaonishitaki, hao wanaosema mabaya juu yangu.


Filipo akamwambia: “Kama unaamini kwa moyo wako wote, unaweza kubatizwa.” Yule mukubwa akamujibu: “Ninaamini kwamba Yesu Kristo ni Mwana wa Mungu.”]


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite