Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Wakorinto 12:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Ni yule yule Roho mumoja anayetenda mambo hayo yote, akimupa kila mumoja zawadi mbalimbali kama anavyopenda.

Gade chapit la Kopi




1 Wakorinto 12:11
18 Referans Kwoze  

Kuna zawadi mbalimbali, lakini ni Roho mumoja anayezitoa.


Mungu vilevile alihakikisha ushuhuda wao kwa njia ya maajabu, ya miujiza mbalimbali, na ya vitambulisho, na kwa njia ya zawadi za Roho Mutakatifu alizowapa watu kama anavyopenda.


Sisi hatutajivuna kupita kipimo, lakini tunataka kutumia kile kipimo cha kazi ile Mungu aliyotupatia na iliyotufikisha vilevile mpaka kwenu.


Lakini kila mutu kati yetu alipokea neema kadiri ya kipimo alichojaliwa na Kristo.


Kuna kazi za namna mbalimbali, lakini Mungu ni mumoja anayewezesha watu wote kuzitimiza.


Kwa mapenzi yake mwenyewe alitupatia sisi uzima kwa njia ya ujumbe wa kweli, kusudi tupate kuwa kama mavuno ya kwanza katikati ya viumbe vyake.


Mungu amefanya kila kitu kufuatana na kusudi na mapenzi yake. Yeye ametuchagua kwa njia ya kuungana kwetu na Kristo, kusudi tukuwe watu wake.


Kwa ngambo ingine, kila mutu aendelee kuishi kufuatana na zawadi aliyopewa na Bwana na kufuatana na vile alivyokuwa mbele ya kuitwa na Mungu. Hii ndiyo kanuni ninayofundisha katika makanisa yote.


Hakika, ningetamani watu wote wakuwe kama mimi, lakini kila mutu amepewa zawadi yake ya kipekee na Mungu, mumoja zawadi hii, na mwingine zawadi ile.


Tuko na zawadi mbalimbali kwa kadiri ya neema tuliyopewa na Mungu. Aliyepewa zawadi ya unabii, anapaswa kutabiri kwa kadiri ya imani yake.


Basi ni kusema kwamba Mungu anamuhurumia yule anayetaka, na kumufanya mugumu yule anayetaka.


Kwa maana kama vile Baba anavyofufua wafu na kuwarudishia uzima, vile vile Mwana anawapa uzima wale anaowataka.


Yoane akawajibu: “Hakuna mutu anayeweza kuwa na kitu isipokuwa amekipewa na Mungu.


Upepo unavuma pahali unapotaka, nawe unasikia sauti yake, lakini haujui pahali unapotoka wala unapokwenda. Na ni vile inavyokuwa kwa kila mutu anayezaliwa kwa Roho.”


Sina haki ya kutumia mali yangu sawa ninavyotaka? Unapatwa na wivu kwa sababu mimi ni mwema?’ ”


Ndiyo, Baba, hayo yote ni kutokana na mapenzi yako.


Lakini sasa, Mungu amepanga viungo vya mwili kila kimoja kama ilivyomupendeza.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite