9 Vilevile tusimupime Bwana kama vile wamoja wao walivyofanya, hata wakauawa na nyoka.
Walimujaribu Mungu kwa makusudi; wakidai wapewe chakula walichotaka.
Pahali pale Musa akapaita “Masa” na “Meriba”, ni kusema “Ujaribu” na “Magombano”, kwa sababu Waisraeli walimugombanisha na kumujaribu Yawe wakisema: “Kweli Yawe yuko pamoja nasi?”
Kwa hiyo watu wakamunungunikia Musa wakisema: “Utupatie maji ya kunywa.” Musa akawauliza: “Mbona munaninungunikia? Mbona munamujaribu Yawe?”
Hata hivyo walimupima na kumwasi Mungu Mukubwa; wala hawakushika maagizo yake.
“Musimujaribu Yawe, Mungu wenu, kama vile mulivyomujaribu huko Masa.
Walipatwa na tamaa kubwa kule katika jangwa, wakamupima Mungu kule kwenye ukiwa.
babu zenu waliponijaribu na kunipima, ingawa walikuwa wameona mambo niliyowatendea.