Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Wakorinto 10:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Musinungunike kama vile wamoja kati yao walivyofanya hata malaika mwangamizaji akawateketeza.

Gade chapit la Kopi




1 Wakorinto 10:10
23 Referans Kwoze  

Wakamunungunikia Musa na Haruni wakisema: Afazali tungekufia Misri! Afazali tungekufia hapahapa katika jangwa!


watu hao waliotoa habari za uongo juu ya hiyo inchi, wakakufa kwa pigo mbele ya Yawe.


Halafu Mungu akatuma malaika aende kuharibu Yerusalema. Lakini mbele hajafanya vile, Yawe akageuza nia yake na kumwambia malaika yule aliyetimiza maangamizi: “Basi, inatosha!” Malaika alikuwa amesimama karibu na uwanja wa kupepetea ngano wa Ornani wa kabila ya Yebusi.


Mufanye kila kitu bila manunguniko wala mabishano,


Lakini wakati malaika aliponyoosha mukono wake kuelekea Yerusalema kwa kuuangamiza, Yawe alibadilisha nia yake. Yawe akamwambia yule malaika aliyetimiza maangamizi kwa watu: “Basi! Inatosha; rudisha mukono wako.” Malaika wa Yawe alikuwa amesimama karibu na kiwanja cha kupepetea ngano cha Arauna wa muji wa Yebusi.


Walinungunika ndani ya hema zao, wala hawakumusikiliza Yawe.


Maana Yawe atapita kuwaua Wamisri. Lakini atakapoona damu iliyopakwa kwenye vizingiti na miimo ya nyumba zenu, atapita na wala hatamuruhusu mwangamizaji kuingia katika nyumba zenu na kuwaua.


Watu hawa wanaendelea kunungunika na kuteta wengine. Wanaishi kufuatana na tamaa zao mbaya. Wanasema maneno ya majivuno na kujipendekeza kwa watu kusudi wapate faida toka kwao.


Basi, watu wote wakamunungunikia Musa wakisema: “Sasa tutakunywa nini?”


Na pale pale malaika wa Bwana akamwazibu Herode kwa ugonjwa kwa sababu alijitukuza kwa pahali pa Mungu. Herode akakuliwa na michango ya tumbo na kisha akakufa.


Naye Yawe akatuma malaika aliyewaua waaskari shujaa, majemadari na wakubwa katika kambi ya mufalme wa Asuria. Basi, mufalme wa Asuria akarudia katika inchi yake akijaa haya. Mara tu alipoingia ndani ya nyumba ya mungu wake, wana wake mwenyewe wakamwua palepale kwa upanga.


Kisha nikasikia sauti kubwa ikitoka katika hekalu ikiwaambia wale wamalaika saba: “Mwende kumwanga vile vikombe saba vya kasirani ya Mungu juu ya dunia!”


Kwa njia ya imani, alianzisha sikukuu ya Pasaka, na kuamuru damu inyunyizwe, kusudi malaika mwangamizaji asiwaue wazaliwa wa kwanza wanaume wa Waisraeli.


Si Haruni tu munayemunungunikia, wewe na kundi lako, lakini kwa kweli munamwasi Yawe.


Hili lilikuwa onyo kwa Waisraeli kwamba mutu yeyote ambaye si kuhani, maana yake asiyekuwa wa ukoo wa Haruni asiende kwenye mazabahu kwa kumufukizia Yawe ubani. Kama sivyo ataangamizwa kama Kora na wafuasi wake. Haya yote yalitendeka kama vile Yawe alivyomwambia Eleazari kwa njia ya Musa.


Ujitenge na watu hawa, niwaangamize mara moja! Lakini wao wakajitupa uso mpaka chini.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite