Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Wakorinto 1:26 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

26 Basi wandugu zangu, mukumbuke vile mulivyoitwa na Mungu, kwamba si wengi kati yenu wenye hekima kufuatana na mafikiri ya watu; si wengi kati yenu wanaokuwa wenye nguvu, wala wenye vyeo.

Gade chapit la Kopi




1 Wakorinto 1:26
24 Referans Kwoze  

Wandugu zangu wapenzi, musikilize: Mungu amewachagua wamasikini wa dunia hii kusudi wakuwe watajiri katika imani, nao wapokee Ufalme ule aliowaahidi wale wanaomupenda.


Hakuna hata mutawala mumoja kati ya watawala wa dunia hii aliyeelewa hekima ile. Kama wangeielewa wasingemutundika Bwana wa utukufu juu ya musalaba.


Basi, tuseme nini juu ya wenye hekima, walimu wa Sheria, nao wafundi wa usemi siku hizi? Mungu ameonyesha wazi kwamba hekima ya dunia hii ni upumbafu!


Saa ile ile, Yesu akajazwa na furaha kwa uwezo wa Roho Mutakatifu, naye akasema: “Ee Baba, Bwana wa mbingu na dunia, ninakushukuru kwa maana mambo uliyoyaficha kwa watu wenye hekima na elimu, umeyafunua kwa wanaokuwa wadogo. Ndiyo Baba, hayo yote ni kutokana na mapenzi yako.


Nasi tunaposema hatutumii maneno yanayotokana na hekima ya kimutu, lakini maneno yanayotokana na Roho wa Mungu, tukieleza maneno ya kiroho kwa watu wanaokuwa wa Roho.


Barua hii inatoka kwangu mimi muzee. Ninakuandikia wewe mama uliyechaguliwa na Mungu, pamoja na watoto wako ninaowapenda hakika. Wala si mimi peke tu ninayewapenda, lakini vilevile wale wote wanaojua ule ukweli wanawapenda ninyi,


Watu wote wa Mungu, na hasa zaidi wale wanaokuwa katika nyumba ya Mufalme, wanawasalimia vilevile.


Ingawa vile watu wamoja walijiunga naye na kuamini. Kati yao kulikuwa Dionisio, mumoja wa Baraza Kubwa inayoitwa Areopago, pamoja na mwanamuke mumoja aliyeitwa Damari na watu wengine vilevile.


Yule liwali alipoona mambo yale yaliyotokea, akashangaa na mafundisho ya Bwana hata akapata kumwamini.


Huyo alitumika pamoja na liwali mumoja mwenye akili, aliyeitwa Sergio Paulo. Liwali huyo akawaita Barnaba na Saulo wafike kwake kwa sababu alitaka kusikia Neno la Mungu.


Nitakuachia watu wapole na wanyenyekevu ambao watakimbilia usalama kwangu mimi Yawe.


Kwa hiyo, watu wote wanamwogopa. Yeye hawajali watu wanaojiona kuwa wenye hekima.


Kwa maana Mungu habadilishi mafikiri juu ya zawadi anazotoa, wala juu ya wale anaowachagua.


Namani alipopata habari hii, akaenda kwa mufalme na kumwelezea habari za mutoto yule.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite