Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Wakorinto 1:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Mungu alikusudia kuwaokoa wale wanaomwamini kwa njia ya mahubiri tunayotangaza yanayoonekana kuwa mambo ya upumbafu. Amefanya vile kwa sababu, kwa njia ya hekima yao ya kimutu, watu hawakumutambua Mungu na hekima yake ya kimungu.

Gade chapit la Kopi




1 Wakorinto 1:21
28 Referans Kwoze  

Saa ile ile, Yesu akajazwa na furaha kwa uwezo wa Roho Mutakatifu, naye akasema: “Ee Baba, Bwana wa mbingu na dunia, ninakushukuru kwa maana mambo uliyoyaficha kwa watu wenye hekima na elimu, umeyafunua kwa wanaokuwa wadogo. Ndiyo Baba, hayo yote ni kutokana na mapenzi yako.


Katika siku zile Yesu akasema: “Ee Baba, Mwenyeji wa mbingu na dunia, ninakushukuru kwa maana mambo uliyoyaficha kwa watu wenye hekima na elimu, umeyafunua kwa wanaokuwa wadogo.


Lakini sasa, kwa njia ya kanisa, watawala na wote wenye uwezo wanaokuwa katika eneo la mbingu wapate kutambua hekima ya Mungu inayokuwa ya namna nyingi.


Lakini kwa wale walioitwa na Mungu, ikiwa Wayuda au wasiokuwa Wayuda, Kristo ni kitambulisho cha uwezo na hekima ya Mungu.


akasema: Jina la Mungu litukuzwe milele na milele. Hekima na nguvu ni vyake.


Hivi kufuatana na vile walivyokataa kumutambua Mungu, Mungu akawaacha wafuate akili yao ya upotevu, kusudi wafanye mambo wasiyopaswa kufanya.


Utajiri wa Mungu, hekima na ufahamu wake ni vikubwa kupita kipimo! Hakuna anayeweza kuvumbua kusudi lake wala kuelewa mipango yake!


“Musiogope ninyi kundi dogo! Kwa kuwa Baba yenu amependelea kuwapa ninyi ule Ufalme wake.


Sasa ni wakati wa dunia hii kuhukumiwa; sasa mutawala wa dunia hii atashindwa.


Hivi, mahubiri ya kufa kwa Kristo juu ya musalaba yanahesabiwa kuwa upumbafu kwa wale wanaopotea. Lakini kwa sisi tunaookolewa ni uwezo wa Mungu.


Lakini sisi tunamuhubiri Kristo aliyetundikwa juu ya musalaba, na mahubiri hayo yanahesabiwa kama kikwazo kwa Wayuda na upumbafu kwa watu wa mataifa mengine.


Kwa maana mambo wanayomuhesabilia Mungu kuwa ya upumbafu, yanapita hekima ya watu; nayo mambo yale wanayomuhesabilia kuwa ya uzaifu yanapita nguvu za watu.


Lakini Mungu anachagua vitu ambavyo watu wanahesabu kuwa vya upumbafu kusudi apatishe wenye hekima haya, naye amechagua vitu wanavyohesabu kuwa vya uzaifu kusudi apatishe wenye nguvu haya.


Lakini mutu anayefuata hali yake ya kidunia hawezi kukubali maneno yanayotoka kwa Roho yule. Kwa sababu anayaona kuwa ni upumbafu kwake, naye hawezi kuyaelewa kwa maana yanatambulikana tu kwa njia ya Roho.


Sisi ni wapumbafu kwa ajili ya Kristo, lakini ninyi ni wenye hekima katika kuungana kwenu na Kristo. Sisi ni zaifu, lakini ninyi ni wenye nguvu. Tunazarauliwa, lakini ninyi munaheshimiwa!


Hamujui kwamba watu wa Mungu ndio watakaohukumu dunia? Na kama ikiwapasa kuhukumu dunia, hamuwezi hata kuhukumu mambo ya burebure?


Lakini tunahukumiwa na kuazibiwa na Bwana kusudi tusiazibiwe pamoja na watu wa dunia hii.


Lakini, Mungu aliyenichagua mbele sijazaliwa na kuniita kwa neema yake, alipendezwa


Zamani, mulipokuwa hamumujui Mungu, mulikuwa watumwa wa miungu isiyokuwa ya kweli.


Ametujulisha mipango yake iliyokuwa imefichwa; ndiyo ile aliyokusudia kwa mapenzi yake tangu mbele kwamba ataitimiza kwa njia ya Kristo.


Kwa maana Mungu mwenyewe alitaka ukamilifu wake uonekane ndani ya mwana wake.


Malaika ni nini, basi? Wao wote ni roho wanaomutumikia Mungu na wanaotumwa naye kwa ajili ya faida ya wale wanaopaswa kuokolewa.


Basi, namna gani sisi tutaponyoka azabu kama hatushuguliki na wokovu mukubwa kama huu? Ni Bwana mwenyewe aliyetangaza kwanza habari za wokovu huu, na wale waliomusikia walihakikisha kwetu kwamba ni za kweli.


Ni kwa sababu hii anaweza kuwaokoa kabisa wao wanaokuja kwa Mungu kwa njia yake, kwa maana yeye anaishi siku zote kusudi akuwe mwombezi mbele ya Mungu.


Ninyi watu wasiokuwa na uaminifu! Hamujui kwamba kupenda raha ya dunia ni kuwa adui wa Mungu? Basi yeye anayetaka kupenda raha za dunia anajifanya mwenyewe kuwa adui wa Mungu.


Nao wakiomba kwa imani, mugonjwa yule atapona, kwa kuwa Bwana atamurudishia afya yake. Na ikiwa amefanya zambi, atasamehewa.


mukumbuke neno hili: yule anayemurudisha mwenye zambi toka njia ya upotevu ataokoa roho ya yule kutoka kifo, na zambi nyingi zitasamehewa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite