Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Wakorinto 1:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Kristo hakunituma kwa kubatiza, lakini amenituma kwa kutangaza Habari Njema. Amenituma kuitangaza bila kutumia hekima ya usemi, kusudi uwezo unaotokana na kufa kwa Kristo juu ya musalaba usihesabiwe kuwa bure.

Gade chapit la Kopi




1 Wakorinto 1:17
13 Referans Kwoze  

Wandugu zangu, wakati nilipokuja kwenu kuwapasha habari ya siri ya Mungu, sikutumia maneno magumu wala hekima ya dunia.


Nasi tunaposema hatutumii maneno yanayotokana na hekima ya kimutu, lakini maneno yanayotokana na Roho wa Mungu, tukieleza maneno ya kiroho kwa watu wanaokuwa wa Roho.


Basi, wakati tulipowajulisha uwezo na kurudia kwa Bwana wetu Yesu Kristo, sisi hatukutumia hadisi za uongo zilizotungwa kwa werevu. Lakini tulijionea na macho yetu sisi wenyewe uwezo wake.


Kwa sababu wengi wanasema: “Barua za Paulo ni kali na zenye maneno mazito; lakini yeye mwenyewe anapokuwa katikati yetu ni muzaifu na namna yake ya kusema ni ya kuzarauliwa.”


Tumekataa mambo ya kisirisiri na ya haya. Hatuna mwenendo wa udanganyifu wala hatupotowi neno la Mungu. Lakini tunajulisha waziwazi ukweli kusudi tuvute kila mutu kutuaminia katika zamiri yake mbele ya Mungu.


(Hakika Yesu mwenyewe hakubatiza mutu lakini ni wanafunzi wake.)


Inaonekana kuwa mimi si mutu anayeelewa kusema, lakini kwa ngambo ya elimu, mimi ninaielewa sana. Nasi tumeonyesha hayo yote kila wakati na katika mambo yote.


Basi akaamuru wabatizwe kwa jina la Yesu Kristo. Na kisha wakamusihi Petro akae kule kwao kwa siku chache.


Yesu akatambua kwamba Wafarisayo wamepata habari kama yeye anapata wanafunzi wengi zaidi kuliko Yoane na kuwabatiza.


Jambo ambalo tunajivunia ni hili: zamiri yetu inayotuhakikishia kwamba tumeishi katika dunia na zaidi kati yenu katika uaminifu na ukweli tulivyojaliwa na Mungu. Sisi hatukuongozwa na hekima ya kimutu lakini na neema ya Mungu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite