Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Wakorinto 1:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Kwa maana, wandugu zangu, nimepata habari zenu kwa njia ya jamaa ya Kloe kwamba kuko ugomvi katikati yenu.

Gade chapit la Kopi




1 Wakorinto 1:11
19 Referans Kwoze  

yeye anajaa majivuno wala hajui kitu. Yeye yuko na ulema wa kubishana na kugombezana juu ya maana ya maneno. Na hayo yanaleta wivu, makelele, matukano, masingiziano


Tusijivune, tusichokozane wala kuoneana wivu.


kwa sababu mungali munatawaliwa na mambo ya kidunia. Kwa maana ikiwa kungali wivu na ugomvi katikati yenu, haionyeshi kwamba munatawaliwa na mambo ya kidunia, nanyi munaishi kufuatana na hali ya kimutu?


Maneno ya mupumbafu yanaleta ugomvi; kila neno analosema linasababisha azabu.


kutambikia sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, kasirani, mapingano, matengano, ubaguzi,


Lakini kama mukiumana na kukulana kama nyama wa pori, muangalie vizuri musiteketezane.


Kwa maana ninaogopa kwamba wakati ninapokuja kwenu, sitawakuta sawa vile ninavyotaka, nanyi hamutanikuta sawa vile munavyotaka. Ninaogopa kuwakuta katika fitina, wivu, kasirani, ugomvi, masingiziano, matetano, majivuno na fujo.


Kiburi kinasababisha tu ugomvi, lakini kwa wanaokubali shauri jema kuna hekima.


Hizi ndizo habari za ukoo wa Yakobo. Yosefu, akiwa kijana wa umri wa miaka kumi na saba, alikuwa akichunga kondoo na mbuzi pamoja na wandugu zake, wana wa Biliha na Zilpa, wake za baba yake. Yosefu akakuwa anamujulisha baba yake juu ya tabia mbaya za wandugu zake.


Lakini Rebeka alipojua nia ya mwana wake mukubwa, akamwita mwana wake mudogo Yakobo, akamwambia: “Angalia, ndugu yako Esau anajifariji akikusudia kukuua.


Mufanye kila kitu bila manunguniko wala mabishano,


Kwanza, ninasikia kwamba munapokusanyika kuna matengano katikati yenu, nami ninasadiki kwamba nusu ya maneno yale ni ya kweli.


Wandugu zangu, ninawasihi ninyi kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo, mukuwe na masikilizano kusudi matengano yasikuwe katikati yenu. Muishi katika umoja kabisa mukiwa na nia moja na wazo moja.


Ninataka kusema: kila mumoja kati yenu anasema maneno yake mbalimbali. Mumoja anasema: “Mimi ni wa Paulo,” mwingine anasema: “Mimi ni wa Apolo,” mwingine anasema: “Mimi ni wa Petro,” na mwingine anasema: “Mimi ni wa Kristo.”


Lakini uepuke mabishano ya upumbafu, hadisi za vizazi vya babu, na magomvi pamoja na mapingano juu ya Sheria, kwa sababu mambo hayo hayana mafaa, nayo ni ya bure.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite