Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Wafalme 2:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 “Mwana wangu, kama inavyokuwa kawaida kwa viumbe vyote kufa, siku zangu zimekwisha. Ukuwe imara na hodari.

Gade chapit la Kopi




1 Wafalme 2:2
21 Referans Kwoze  

“Sasa, wakati wangu wa kufa kama inavyokuwa kawaida ya wanadamu wote umekaribia. Lakini ninyi wote munajua wazi ndani ya mioyo na roho zenu kwamba katika mambo yote mema ambayo Yawe, Mungu wenu aliwaahidi, hakuna hata moja ambalo halikutimia. Yote yametimia kama vile alivyoahidi.


Basi kwa kumaliza, musimame imara katika kuungana kwenu na Bwana kwa uwezo wa nguvu zake kubwa.


Mukeshe, musimame imara katika imani, mukuwe hodari na wenye nguvu.


Kila mutu anapaswa kufa mara moja tu, na nyuma ya kufa, anahukumiwa na Mungu.


Kisha Yawe akamwagiza Yoshua, mwana wa Nuni, akamwambia: “Ukuwe imara na hodari, maana utawaongoza Waisraeli katika inchi ambayo nimewaapia kuwapa, nami nitakuwa pamoja nawe.”


Basi wewe mwana wangu, ukuwe hodari kwa njia ya neema uliyopata katika kuungana kwako na Kristo Yesu.


Usijiachilie kuzarauliwa na mutu yeyote kwa sababu ungali bado kijana. Lakini ukuwe mufano kwa waamini, katika masemi yako, katika mwenendo wako, katika upendo, katika imani na katika maisha safi.


Nyuma ya hayo yote yaliyokwisha kusemwa, kungali hili linalotakiwa: Umwogope Mungu, na ushike amri zake, kwa sababu hayo ndiyo mapaswa ya mwanadamu.


Unikumbuke, ee Bwana. Maisha ni mafupi! Umewaumba wanadamu wote kwa bure?


Kweli! Ninajua utanipeleka tu katika kifo, pahali wote wanaoishi watakapokutana.


Kweli, miaka yangu ni michache, nami nitakwenda kule ambako sitarudi.


Kisha, mufalme Daudi akamwambia Solomono mwana wake: “Uwe imara na hodari, ufanye kazi hii. Usiogope wala kuwa na wasiwasi. Yawe Mungu ambaye ni Mungu wangu, yuko pamoja nawe. Hatakuachilia lakini atakuwa nawe mpaka itakapomalizika kazi yote ambayo inayohitajika kufanyiwa kwa nyumba ya Yawe.


Ee Yawe, Mungu wangu, umeniweka mimi mutumishi wako kuwa mufalme pahali pa baba yangu Daudi, ijapokuwa ningali mutoto mudogo na sijui namna ya kutimiza kazi hii.


Lakini ujipe moyo! Tupigane kama wanaume kwa ajili ya watu wetu na kwa ajili ya miji ya Mungu wetu. Naye Yawe atutendee lile analoona ni jema kwake.”


Lakini sasa amekufa, kwa nini nifunge? Mimi ninaweza kumurudisha katika dunia? Siku moja, nitakwenda kule alikokwenda, lakini yeye hawezi kurudi kwangu.”


Ukiwa mwangalifu, na ukitii masharti na maagizo ambayo Yawe alimwagiza Musa juu ya Israeli, utastawi. Ujipe moyo, ukuwe imara. Usiogope wala usifazaike.


wa kufua zahabu, feza, shaba na chuma. Basi sasa, anza kazi! Yawe akuwe pamoja nawe!”


Basi fanya angalisho na kukumbuka kwamba Yawe amekuchagua wewe umujengee nyumba ya ibada. Ukuwe hodari na utende hivyo.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite