Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Wafalme 1:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Wakati ule, Adonia mwana wa Daudi kutoka muke wake Hagiti, akaanza kujivuna kwamba yeye ndiye atakayekuwa mufalme. Basi, akajitayarishia magari, wapanda-farasi na watu makumi tano wa kumutangulia.

Gade chapit la Kopi




1 Wafalme 1:5
19 Referans Kwoze  

Nyuma ya tukio hilo, Abusaloma alijipatia gari, farasi na watu makumi tano wa kumutangulia.


Adonia muzaliwa wa ine, mama yake alikuwa Hagiti; Sefatia muzaliwa wake wa tano, mama yake alikuwa Abitali;


Yesu akaongeza kusema: “Ninawaambia kwamba mutu huyu alirudia kwake akiwa amehesabiwa kuwa na haki mbele ya Mungu, lakini si yule Mufarisayo. Kwa maana kila mutu anayejiinua atashushwa, lakini anayejishusha atainuliwa.”


Kwa maana kila mutu anayejiinua atashushwa, lakini anayejishusha atainuliwa.”


Inchi yao imejaa feza na zahabu, akiba yao ni kubwa zaidi. Inchi yao imejaa farasi, magari yao ya vita hayana hesabu.


Majivuno ya ndani ya moyo yanaleta maangamizi, lakini unyenyekevu unaleta heshima.


Kiburi kinatangulia maangamizi; majivuno yanatangulia maanguko.


Mufalme Daudi akawaambia wale watu wote waliokusanyika: “Solomono mwana wangu, ambaye peke yake amechaguliwa na Mungu, angali bado mudogo, hana maarifa mengi na kazi hii ni kubwa. Nyumba atakayojenga si ya mwanadamu, lakini ni ya Mungu, Yawe.


Yawe amenijalia wana wengi, na kati ya hao wote, amemuchagua Solomono mwana wangu, aikae juu ya kiti cha kifalme cha ufalme wa Yawe atawale.


Sasa basi, kama vile Yawe anavyoishi, yule aliyeniweka na kuniimarisha katika ufalme wa baba yangu Daudi na kutimiza ahadi yake ya kunipa kiti cha kifalme mimi na wazao wangu, Adonia atakufa leo!”


Kisha, Natani akamwendea Batiseba mama ya Solomono, akamwuliza: “Haujasikia kwamba Adonia mwana wa Hagiti amejiweka kuwa mufalme na bwana wetu Daudi hana habari?


Lakini ungali unaonyesha kiburi juu ya watu wangu, wala hauwaachi waondoke.


“Museme hapa hapa mbele ya wanainchi wote wa Sekemu: Jambo gani ni jema kwenu, kwamba watoto wote makumi saba wa kiume wa Yerubali wawatawale au mutoto mumoja? Mukumbuke kwamba mimi ni damu yenu.”


Binti yule, alikuwa muzuri sana. Basi, akaanza kumutumikia na kumutunza mufalme, lakini mufalme hakumujua kimwili.


Adonia akamwambia: “Unajua kwamba ni mimi ndiye ningalikuwa mufalme, na hata Israeli yote ilikuwa inanitazamia nikuwe mufalme. Lakini, mambo yakageuka na ndugu yangu akanipindua, kwa sababu hayo ndiyo yaliyokuwa mapenzi ya Yawe.


Nyuma, Adonia mwana wa Hagiti, alimwendea Batiseba, mama ya Solomono. Batiseba akamwuliza: “Unaleta habari ya amani?” Adonia akamujibu: “Ndiyo, ninaleta habari ya amani.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite