Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Wafalme 1:36 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

36 Benaya mwana wa Yehoyada akamujibu mufalme: “Amina! Yawe, Mungu wa bwana wangu mufalme, aseme vile vile.

Gade chapit la Kopi




1 Wafalme 1:36
16 Referans Kwoze  

Kwa maana kama ukimwomba Mungu ndani ya roho tu kwa kumushukuru, mutu asiyeelewa kitu anayehuzuria katika mukutano hawezi kusema amina kwa kuitikia maombi yako ya kushukuru. Ni kwa sababu hasikii mambo unayosema.


Muwafundishe kutii maneno yote niliyowaagiza. Na mujue kwamba mimi ni pamoja nanyi siku zote hata mwisho wa dunia.”


Usituache kuanguka katika majaribu, lakini utuokoe na yule Mwovu. [Kwa maana ufalme, uwezo na utukufu ni vyako hata milele. Amina.]’


Ikuwe hivyo! Yawe afanye hivyo. Yawe ayatimize maneno uliyotabiri, avirudishe hapa vyombo vya nyumba ya Yawe kutoka Babeli pamoja na watu wote waliohamishiwa huko.


Na kwa njia hiyo mimi nitatimiza ahadi niliyowatolea babu zenu, kwamba nitawapa inchi inayojaa maziwa na asali, kama inavyokuwa hata leo. Nami nikajibu: Ikuwe hivyo, ee Yawe.


Nitaongeza nguvu na utawala wake, kutoka bahari ya Mediteranea mpaka muto Furati.


Zamani ulisema katika maono, ukawaambia watumishi wako waaminifu: “Nimemupa nguvu shujaa mumoja, nimemwinua huyo niliyemuchagua kati ya watu.


Jina lake tukufu litukuzwe milele; utukufu wake ujae katika ulimwengu wote! Amina, Amina!


Zaburi ya Daudi wakati alipokuwa katika jangwa la Yudea.


Ninakupenda, ee Yawe, nguvu yangu!


Kwa hiyo ninakuomba ubariki wazao wangu, mimi mutumishi wako, kusudi wadumu milele mbele yako; maana unapobariki, baraka zako zinadumu milele.”


Kukitokea watu wanaokufuatilia na kutaka kuyaangamiza maisha yako, Yawe, Mungu wako, atayalinda maisha yako pamoja na watu wanaokuwa wazima. Lakini atayatupilia mbali maisha ya waadui zako, kama vile mutu anavyotupa jiwe kwa mujeledi.


Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa kiongozi wa Wakereti na Wapeleti. Wana wa Daudi wakakuwa makuhani.


Nanyi mutamufuata, naye atakuja na kuikaa juu ya kiti changu cha kifalme kwa pahali pangu; nami nimemuchagua kuwa mutawala juu ya Israeli na juu ya Yuda.”


Kama Yawe alivyokuwa pamoja na bwana wangu mufalme, akuwe vilevile na Solomono, na akitukuze kiti chake cha kifalme kuliko kiti cha kifalme cha bwana wangu mufalme Daudi.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite