Kwa maana kama ukimwomba Mungu ndani ya roho tu kwa kumushukuru, mutu asiyeelewa kitu anayehuzuria katika mukutano hawezi kusema amina kwa kuitikia maombi yako ya kushukuru. Ni kwa sababu hasikii mambo unayosema.
Ikuwe hivyo! Yawe afanye hivyo. Yawe ayatimize maneno uliyotabiri, avirudishe hapa vyombo vya nyumba ya Yawe kutoka Babeli pamoja na watu wote waliohamishiwa huko.
Na kwa njia hiyo mimi nitatimiza ahadi niliyowatolea babu zenu, kwamba nitawapa inchi inayojaa maziwa na asali, kama inavyokuwa hata leo. Nami nikajibu: Ikuwe hivyo, ee Yawe.
Kukitokea watu wanaokufuatilia na kutaka kuyaangamiza maisha yako, Yawe, Mungu wako, atayalinda maisha yako pamoja na watu wanaokuwa wazima. Lakini atayatupilia mbali maisha ya waadui zako, kama vile mutu anavyotupa jiwe kwa mujeledi.
Nanyi mutamufuata, naye atakuja na kuikaa juu ya kiti changu cha kifalme kwa pahali pangu; nami nimemuchagua kuwa mutawala juu ya Israeli na juu ya Yuda.”
Kama Yawe alivyokuwa pamoja na bwana wangu mufalme, akuwe vilevile na Solomono, na akitukuze kiti chake cha kifalme kuliko kiti cha kifalme cha bwana wangu mufalme Daudi.”