Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Wafalme 1:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Umwendee mufalme Daudi, umwulize: ‘Bwana wangu mufalme, si uliniapia mimi mujakazi wako ukisema: Mwana wako Solomono atatawala nyuma yangu, na ataikaa juu ya kiti changu cha kifalme? Imekuwa namna gani basi, sasa Adonia anatawala?’

Gade chapit la Kopi




1 Wafalme 1:13
16 Referans Kwoze  

kama nilivyokuapia mbele ya Yawe, Mungu wa Israeli, nikisema: ‘Mwana wako Solomono atatawala nyuma yangu, na ataikaa juu ya kiti changu cha kifalme pahali pangu’, ndivyo nitakavyofanya leo.”


Batiseba akamujibu: “Bwana wangu, uliniapia mimi mujakazi wako mbele ya Mungu wako Yawe, ukisema: ‘Mwana wako Solomono atatawala nyuma yangu, na ataikaa juu ya kiti changu cha kifalme.’


ndivyo itakuwa kwa agano nililofanya na mutumishi wangu Daudi. Nilifanya agano na Daudi kwamba atakuwa na mumoja wa uzao wake wa kutawala pahali pake siku zote; vilevile kutakuwa makuhani wa ukoo wa Lawi watakaonitumikia siku zote.


Yawe ametoa neno juu ya Yakobo nalo litamupata Israeli.


Halafu Solomono akaikaa katika kiti cha kifalme cha Yawe, kwa pahali pa baba yake Daudi. Naye akafanikiwa; na taifa lote la Waisraeli likamutii. 29.23 Ang. 1 Fal 2.12


Basi, Solomono akaikaa katika kiti cha kifalme kwa pahali pa baba yake Daudi, na ufalme wake ukaimarika.


na kuomba akisema: ‘Asifiwe Yawe, Mungu wa Israeli, ambaye amemufanya muzao wangu kuwa mufalme kwa pahali pangu, na ambaye amenipa maisha hata nimeyaona mambo hayo.’ ”


Halafu Natani akasema: “Bwana wangu mufalme, ni kweli kwamba ulisema hivi: ‘Adonia atatawala nyuma yangu, na ataikaa juu ya kiti changu cha kifalme’?


Kisha, Natani akamwendea Batiseba mama ya Solomono, akamwuliza: “Haujasikia kwamba Adonia mwana wa Hagiti amejiweka kuwa mufalme na bwana wetu Daudi hana habari?


Nanyi mutamufuata, naye atakuja na kuikaa juu ya kiti changu cha kifalme kwa pahali pangu; nami nimemuchagua kuwa mutawala juu ya Israeli na juu ya Yuda.”


Atakapokuwa akiikalia kiti cha ufalme anapaswa kuandika mufano wa sheria hii katika kitabu kinachokuwa mbele ya makuhani wa Kilawi.


Na utakapokuwa ungali unaongea na mufalme, mimi nitaingia na kuyahakikisha maneno yako.”


Yawe amenijalia wana wengi, na kati ya hao wote, amemuchagua Solomono mwana wangu, aikae juu ya kiti cha kifalme cha ufalme wa Yawe atawale.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite