Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Timoteo 6:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Watu wote wanaokuwa watumwa wanapaswa kuwaheshimu wabwana wao kabisa, kusudi watu wasitukane jina la Mungu na kuzarau mafundisho yetu.

Gade chapit la Kopi




1 Timoteo 6:1
35 Referans Kwoze  

na kuwa wenye utaratibu, wenye maisha safi, wenye kutunza nyumba zao vizuri, wema na wenye kutii waume wao, kusudi Neno la Mungu lisitukaniwe.


Kwa maana kama ilivyoandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Kwa sababu yenu, jina la Mungu linatukaniwa katikati ya watu wa mataifa mengine.”


mukiwa na zamiri safi, hata wale wanaowasingizia na kuwatukana juu ya mwenendo wenu muzuri katika ushirika wenu na Kristo, wapate haya.


Mukuwe na mwenendo muzuri kati ya wapagani, kusudi wakiwasingizia kwamba mumefanya mabaya, wapate kuona matendo yenu mema na wamutukuze Mungu siku ile ya kuja kwake.


Kristo ametukomboa katika utumwa kusudi tukuwe huru kabisa. Basi, musimame imara wala musijitie tena katika vifungo vya utumwa.


Basi sasa, kwa nini munataka kumupima Mungu kwa kuwabebesha muzigo ambao wala babu zetu, wala sisi wenyewe hatukuweza kuubeba?


Nao wakamujibu: “Tumetumwa hapa na Kornelio, mukubwa wa waaskari. Yeye ni mutu wa haki na mwenye kumutii Mungu, naye anasifiwa na Wayuda wote. Malaika mutakatifu amemutokea na kumwagiza akuite ufike kwake kusudi asikie maneno utakayomwambia.”


Yule malaika aliyesema na Kornelio alipoondoka, akawaita watu wawili kati ya watumishi wake na askari mumoja mwenye kuogopa Mungu, aliyekuwa mumoja wa wasimamizi wake wa kipekee.


Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Sherti mambo ya kuwaangusha watu yatokee, lakini ole kwa mutu yule anayeyaleta!


Nira yangu si nzito, nao muzigo nitakaowabebesha ni mwepesi.”


Yawe wa majeshi anasema hivi: Mutoto anamuheshimu muzazi wake, na mutumishi anamuheshimu bwana wake. Ikiwa mimi ndiye Baba wenu, mbona munanivunjia heshima? Ikiwa mimi ni bwana wenu, mbona hamuniheshimu? Ninasema hivyo kwa ninyi makuhani munaozarau jina langu. Nanyi munauliza: Sisi tumezarau jina lako namna gani?


Kwa sababu hiyo, ninataka wajane wanaokuwa wangali vijana waolewe, wazae watoto na kutunza nyumba zao, kusudi waadui wasipate nafasi ya kutuchongea.


Basi muangalie, kusudi musiwakwaze Wayuda, wala wasiokuwa Wayuda, wala kanisa la Mungu.


Basi mulikwenda kuona nini? Nabii? Ndiyo, ninawaambia, yeye ni mukubwa kupita hata nabii.


Nitalitakasa jina langu kubwa mulilokufuru kati ya mataifa. Na kwa hiyo mataifa yatatambua kwamba mimi ni Yawe. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.– Nitawatumia ninyi kuonyesha utakatifu wangu mbele yao.


Hata walipokuwa kati ya mataifa walilikufuru jina langu takatifu, hata watu wakasema hivi juu yao: Hawa ndio wale watu wa Yawe, lakini wamelazimishwa kuondoka katika inchi yake!


Mafungo ninayotaka mimi ni haya: kuwafungua waliofungwa bila haki, kuziondoa kamba za utumwa, kuwaacha huru wanaogandamizwa, na kuvunja kabisa mambo yote ya kitumwa!


Katika hali ya sasa ninapata faida gani kuwaona watu wangu wamepelekwa katika utumwa? –Ni ujumbe wa Yawe. Hao wanaowatawala wanajitapa. Nalo jina langu linaendelea kuzarauliwa kila siku. –Ni ujumbe wa Yawe.


Niliwakasirikia watu wangu, Israeli, nikawafanya watu wangu kuwa wanaharamu. Niliwatia katika mikono yako, nawe haukuwaonea huruma; na wazee uliwabebesha nira nzito sana.


Walawi, ni kusema Yesua, Kadimieli, Bani, Hasabuea, Serebia, Hodia, Sebania na Petahia, wakawaambia watu: Musimame na kumusifu Yawe, Mungu wenu. Mumusifu milele na milele! Na watu wakasifu jina lako tukufu, ambalo linatukuka kuliko baraka na sifa zote.


Watumishi wake wakamwendea na kumwambia: “Baba yetu, kama nabii angekuambia ufanye jambo fulani gumu, haungelifanya? Sasa, aliyokuambia tu ni: ‘Ujioshe, kusudi upone!’ ”


Hata hivyo, kwa sababu kwa tendo lako umemuzarau kabisa Yawe, mutoto wako atakufa.”


Kwa hiyo mutawatumikia waadui zenu ambao Yawe atawatuma mbele yenu, kwa njaa, kiu na uchi, na ukosefu wa kila kitu. Atawafunga nira ya chuma mpaka awaangamize.


akisema: “Atukuzwe Yawe, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, ambaye hajasahau wema na uaminifu wake kwa bwana wangu. Yawe ameniongoza mimi mwenyewe moja kwa moja mpaka kwa jamaa ya bwana wangu!”


Naye akaomba: “Ee Yawe, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, ninakuomba unisaidie leo na umutendee mema bwana wangu Abrahamu.


Siku moja Abrahamu akamwambia mutumishi wake aliyekuwa muzee kuliko wengine na musimamizi wa mali yake yote: “Weka mukono wako chini ya paja yangu,


Yule malaika wa Yawe akamwambia: “Rudi kwa bibi mukubwa wako Sarai na umutii.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite