Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Timoteo 5:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Uwaheshimu wanawake wajane wasiokuwa na tegemeo lolote.

Gade chapit la Kopi




1 Timoteo 5:3
28 Referans Kwoze  

“ ‘Alaaniwe mutu yeyote anayepotosha haki ya mugeni au yatima au mujane’. Na watu wote wataitika: ‘Amina!’


Katika siku zile, kufuatana na jinsi hesabu ya wanafunzi wa Yesu ilivyokuwa ikizidi kuongezeka, kulitokea manunguniko kati ya Wayuda waliosema Kigriki na Wayuda waliosema Kiebrania. Wale waliosema Kigriki walinungunika kwa sababu wajane wao walisahauliwa wakati wa kugawanya vifaa vya kila siku.


Hiyo itakuwa kwa ajili ya Walawi, kwa sababu hawana fungu wala urizi wao kati yenu, nao wageni, wayatima na wajane ambao wanaishi katika miji yenu, watakuja kula na kushiba. Mufanye hivi naye Yawe, Mungu wenu, atawabariki katika kazi zenu zote munazofanya kwa mikono yenu.


Anatetea haki ya wayatima na wajane; vilevile anawapenda wageni na kuwapa chakula na nguo.


Muwaheshimu watu wote. Muwapende wandugu zenu waamini. Mumwogope Mungu, mumuheshimu mufalme.


Mutafanya karamu hiyo, ninyi na watoto wenu wanaume na wanawake, watumishi wenu, Walawi, wageni, wayatima na wajane ambao wanaishi katika miji yenu.


Mutafurahia mbele ya Yawe, Mungu wenu, ninyi pamoja na wana wenu na wabinti zenu, watumishi wenu, Walawi, wageni, wayatima na wajane ambao wanaishi pamoja nanyi. Mufanye haya katika pahali Yawe, Mungu wenu, atakapochagua kwa ajili ya jina lake.


Uwaheshimu baba yako na mama yako, kusudi uishi maisha marefu katika inchi ninayokupatia mimi Yawe, Mungu wako.


Vilevile, ninyi waume, mukae na wake wenu mukifahamu kwamba wao ni kiumbe kizaifu. Munapaswa vilevile kuwapa heshima kwa sababu watapokea pamoja nanyi zawadi ya uzima. Mufanye hivi kusudi maombi yenu yasizuizwe.


Dini inayokuwa safi na bila kosa mbele ya Mungu Baba ndiyo hii: kushugulikia wayatima na wajane wanaoteswa, na kujilinda mwenyewe na uchafu wa dunia hii.


Hatukutafuta sifa ya watu wala yenu, wala ya mutu mwingine yeyote,


Mara moja Petro akaenda pamoja nao. Naye alipofika wakamupeleka ndani ya chumba cha gorofi. Wajane wote wakamuzunguka Petro, wakilia na kumwonyesha kanzu na nguo zote Dorika alizowashonea wakati alipokuwa angali muzima.


Alipokaribia kwenye mulango wa ukuta wa muji, kukatokea watu wanaobeba maiti ya kijana mumoja aliyekuwa mutoto wa pekee wa mama mumoja mujane. Nao watu wengi wa muji ule walikuwa wakimusindikiza yule mama.


Kisha akabaki mujane, hata akaeneza umri wa miaka makumi nane na mine. Alibaki katika hekalu, akitumikia Mungu usiku na muchana, akifunga kula chakula na kuomba.


“Ole kwenu, ninyi walimu wa Sheria na Wafarisayo, ninyi wanafiki! Munawafungia watu wengine njia ya kuingia katika Ufalme wa mbinguni. Ninyi wenyewe hamwingii mule na zaidi ya hii munawazuiza wale wanaotaka kuingia. [


basi, hapaswi tena kumusaidia baba yake. Hivi munazarau Neno la Mungu kwa kufuata desturi zenu.


Muniachie watoto wenu wayatima nami nitawatunza; muwaache wajane wenu wanitegemee.


Yawe anawalinda wageni, anawasaidia wajane na wayatima; lakini anaharibu mipango ya waovu.


Wanaua wajane na wageni; wanachinja wayatima.


Mumwimbie Mungu, musifu jina lake; mumutengenezee njia yeye anayetembea juu ya mawingu. Jina lake ni Yawe; mufurahi mbele yake.


Nimepata kumukatalia masikini mahitaji yake au kuwafanya wajane watumaini bure?


Waliokuwa karibu kuangamia walinitakia baraka. Niliwafanya wajane waone tena furaha ndani ya moyo.


nao wanawake wazee kama mama yako na vijana wanawake kama wadada zako, ukijilinda katika maisha safi.


Wakati Yesu alipomwona Natanaeli akikuja kwake akasema hivi juu yake: “Angalia Mwisraeli wa kweli asiyekuwa na udanganyifu ndani yake hata kidogo!”


Petro akamushika mukono na kumusimamisha wima. Kisha akawaita wanafunzi na wajane, akamupeleka mbele yao akiwa muzima.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite