Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Timoteo 4:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Wao wanafundisha kwamba ni vibaya kuoana, na wanawakataza watu kula vyakula fulani fulani. Lakini Mungu aliumba vyakula vile kusudi watu waliokwisha kumwamini na kutambua ukweli wapate kuvitumia wakisha kumushukuru.

Gade chapit la Kopi




1 Timoteo 4:3
30 Referans Kwoze  

Kila kitu Mungu alichokiumba ni kizuri, wala hakuna kile kinachopaswa kukataliwa, lakini inafaa kumushukuru Mungu mbele ya kukikula.


Ndoa inapaswa kuheshimiwa na watu wote, mume na muke wake wanapaswa kujikinga na uchafu, kwa sababu Mungu atawahukumu wazinzi na waasherati.


Mutu yeyote anayeshugulika juu ya siku fulani, anafanya hivi kwa kumutukuza Bwana. Yule anayekula kila chakula, anafanya vile kwa kumutukuza Bwana; maana anamushukuru Mungu kwa ajili ya chakula chake. Na asiyekula kila chakula anafanya hivi vilevile kwa kumutukuza Bwana na kumushukuru Mungu.


Basi, mutu asiwahukumu juu ya chakula au kinywaji, au juu ya kushika sikukuu fulani, ikiwa sikukuu ya Mwandamo wa Mwezi au siku ya Sabato.


Chakula hakitaleta ushirika kati yetu na Mungu. Kama tukiacha kula hatupungukiwi kitu na kama tukikula hatuongezewi kitu.


Nyama wote wenye uzima watakuwa chakula chenu; ninawapa nyama hao kama vile nilivyowapa mimea kuwa chakula chenu.


Kila kitu munachofanya au kusema, mufanye yote kwa jina la Bwana Yesu, kwa kumushukuru Mungu Baba kwa njia yake.


Lakini kama ukioa, haufanyi zambi, na kama binti anaolewa, yeye hafanyi zambi vilevile. Lakini wale wanaooana watakuwa na mateso katika maisha yao, na mimi ninataka kuwaonya kusudi muepuke mateso yale.


Yule anayekula kila chakula asimuzarau yule asiyekula kila chakula. Vilevile yule asiyekula kila chakula asimuhukumu yule anayekikula, kwa maana Mungu amemupokea.


Musidanganywe na mafundisho mengine ya kigeni ya kila namna. Kwa maana mioyo yetu inapaswa kutiwa nguvu kwa njia ya neema ya Mungu, wala si kwa njia ya kushika kanuni zinazoagizwa juu ya vyakula. Kanuni hizo haziwafalii kitu wale wanaozishika.


anayetaka watu wote waokolewe na kuweza kutambua ukweli.


Nanyi munasema vilevile: “Chakula kiliumbwa kwa ajili ya tumbo nayo tumbo kwa ajili ya chakula.” Ndiyo, lakini Mungu ataharibu vyote viwili. Lakini mwili haukuumbwa kwa ajili ya uasherati. Mwili uliumbwa kwa ajili ya Bwana nao ni wake.


Kwa maana kazi ya Ufalme wa Mungu si kushugulika na mambo ya kula na kunywa, lakini ni kushugulika na haki, amani na furaha vinavyotolewa na Roho Mutakatifu.


Kisha akatwaa ile mikate saba na zile samaki, akamushukuru Mungu, akaimega na kuwapa wanafunzi wake wavigawanye kwa watu.


Kama Mungu anamupa mutu utajiri na mali na kumujalia wakati wa kuyafurahia, basi mwanadamu ashukuru na avifaidie hivyo alivyojipatia kwa jasho lake. Hiyo ni zawadi kutoka kwa Mungu.


Kisha kuwaamuru watu waikae juu ya majani, Yesu akatwaa ile mikate mitano na samaki mbili, akainua macho mbinguni, akamushukuru Mungu. Akamega ile mikate, akawapa wanafunzi wake, nao wakaigawanya kwa kundi la watu.


Kisha kusema maneno hayo, Paulo akatwaa mukate, akamushukuru Mungu mbele yao wote, akaumega, na akaanza kula.


Na vilevile vyombo vingine vilivyotoka katika muji Tiberia vilifika karibu na pahali pale walipokula mikate, Bwana alipokuwa amekwisha kushukuru Mungu.


Alipokuwa akiikaa kula chakula pamoja nao, akatwaa mukate na kuubariki. Kisha akaumega na kuwapatia.


Mufalme huyo hataijali miungu ya babu zake wala yule anayependwa na wanawake. Ataizarau miungu mingine yote, maana atajiweka kuwa mukubwa kuliko kila mumoja wao.


Mara moja mutakapoingia katika muji, mutamukuta mbele hajakwenda kwenye nafasi ya ibada kwenye mulima kwa kula. Maana watu hawatakula mpaka kwanza yeye abariki sadaka. Kisha wale walioalikwa watakula. Hivyo muende haraka; mutakutana naye sasa hivi.”


Kitu kinachoingia ndani ya kinywa cha mutu hakiwezi kumuchafua. Lakini ni kile kinachotoka ndani ya kinywa chake ndicho kinachomuchafua.”


Kwa sababu hiyo, ninataka wajane wanaokuwa wangali vijana waolewe, wazae watoto na kutunza nyumba zao, kusudi waadui wasipate nafasi ya kutuchongea.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite