Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Timoteo 4:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Na ni kwa hiyo tunasumbuka na kupigana, kwa maana tunamutumainia Mungu Mwenye Uzima, Mwokozi wa watu wote na hasa zaidi Mwokozi wa waamini.

Gade chapit la Kopi




1 Timoteo 4:10
40 Referans Kwoze  

anayetaka watu wote waokolewe na kuweza kutambua ukweli.


Yeye ndiye sadaka iliyotolewa kwa ajili ya usamehe wa zambi zetu, wala si kwa ajili ya zambi zetu tu, lakini kwa ajili ya zambi za watu wote.


aliyejitoa mwenyewe kusudi awakomboe watu wote. Na huo ni ushuhuda kwa wakati uliopangwa, kwamba Mungu anataka kuwaokoa watu wake.


Kesho yake Yoane akamwona Yesu akikuja kwake, akasema: “Angalia Mwana-Kondoo wa Mungu anayeondoa zambi ya dunia!


Na sisi tumeona na kushuhudia kwamba Baba amemutuma Mwana wake kuwa Mwokozi wa dunia.


nao wakamwambia yule mwanamuke: “Sasa tunaamini, si kwa sababu ya maneno uliyotuambia tu, lakini kwa sababu tumesikia sisi wenyewe na tunajua hakika kwamba huyu ni Mwokozi wa dunia.”


“Kweli, kweli ninawaambia: anayesikia neno langu na kumwamini yule aliyenituma, anapata uzima wa milele. Yeye hatahukumiwa, lakini ameponyoka lufu na kupata uzima.


Yawe Mungu ni jua na ngao yetu. Anatukubali na anatupatia utukufu. Hawanyimi kitu chochote kizuri wale wanaoishi katika ukamilifu.


Basi tumwendee mbali na kambi, tukikubali kuzarauliwa kama vile yeye alivyozarauliwa.


Mungu ndiye mwenye kuniokoa, nitamutegemea yeye, wala sitaogopa; Yawe ananijalia nguvu; yeye mwenyewe ndiye anayeniokoa.


Afazali kumukimbilia Yawe kuliko kumutumainia mwanadamu.


Watu wa haki wataona, wataogopa, na kisha watakuchekelea na kusema:


Kwa njia ya Kristo, ninyi munamwamini Mungu aliyemufufua na kumupa utukufu. Na kutokana na hiyo munamwamini Mungu na kumuwekea tumaini lenu.


Aliona kwamba kupatishwa haya kwa ajili ya Kristo kuna faida kubwa zaidi kuliko kupata utajiri wote wa inchi ya Misri, maana alikuwa anatazamia kupokea zawadi yake.


Uwaagize wale wanaokuwa watajiri katika dunia hii ya sasa wasijivune, vilevile wasiweke matumaini yao katika mali inayotoweka upesi. Lakini wamutumainie Mungu anayetupatia vitu vyote kwa uwingi kusudi tufurahiwe navyo.


Lakini, kama nikikawia kufika, utaweza hivi kujua mwenendo unaopaswa kuwa nao katika nyumba ya Mungu, maana yake katika jamaa ya Mungu Mwenye Uzima. Yeye ndiye anayekuwa nguzo na musingi wa kweli.


Yeye alimutumainia Mungu na alisema kwamba yeye ni Mwana wa Mungu. Ikiwa Mungu anapendezwa naye sasa amwokoe!”


Yawe ni muzuri, yeye ni kimbilio la usalama wakati wa taabu. Yeye anawalinda wote wanaokimbilia usalama kwake.


Basi, mufalme Nebukadneza akasema: Asifiwe Mungu wa Sadiraki, Mesaki na Abedenego kwa sababu alimutuma malaika wake na kuwaokoa watumishi wake ambao wanamutegemea. Wao walikataa kutii amri yangu ya kifalme, wakaitoa miili yao kama sadaka pahali pa kuabudu mungu mwingine, lakini Mungu wao peke yake.


Abarikiwe mutu anayenitegemea mimi Yawe, mutu ambaye mimi Yawe ndiye tegemeo lake.


Nani kati yenu anayemwogopa Yawe? Nani anayetii maneno ya mutumishi wake? Kama kuna mutu anayetembea katika giza bila taa, amutumainie Yawe, na kumutegemea Mungu wake.


Museme hivyo, enyi muliokombolewa na Yawe, watu ambao aliwaokoa katika taabu,


Yawe anawasaidia na kuwaokoa; anawaopoa kutoka makucha ya waovu na kuwaokoa, maana wanakimbilia kwake.


Wema wako, ee Yawe, unaenea hata mbinguni; uaminifu wako unafika hata kwenye mawingu.


Simoni Petro akamujibu: “Wewe ni Kristo, Mwana wa Mungu Mwenye Uzima.”


Lakini kwa neema ya Mungu nimekuwa sawa hivi ninavyokuwa, na neema yake niliyopewa haikukuwa ya bure, lakini nilitumika zaidi sana kuliko mitume wote wengine. Hakika si mimi, lakini ni neema ya Mungu inayokuwa pamoja nami.


Yeye ndiye aliyetuopoa toka hatari kubwa sana ya kufa, naye atatuopoa tena. Nasi tunamutumainia kwamba ataendelea kutuopoa,


Nalo jambo hilo ni zuri na lenye kupendeza Mungu Mwokozi wetu,


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite