Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Timoteo 3:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Vilevile wasaidizi wanaotumika katika kanisa wanapaswa kuwa watu wenye heshima. Hawapaswi kuwa wenye nia mbili katika masemi yao wala wenye kunywa pombe kwa uwingi wala wenye kutafuta mali kwa njia isiyokuwa sawa;

Gade chapit la Kopi




1 Timoteo 3:8
17 Referans Kwoze  

Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo na kwa ndugu yetu Timoteo, sisi watumishi wa Yesu Kristo. Tunawaandikia watu wote wa Mungu wanaoungana na Yesu Kristo, wanaoishi Filipi, pamoja na wazee wa kanisa na wasaidizi.


Vilevile uwaambie wanawake wazee wakuwe na mwenendo unaostahili kwa watu watakatifu. Hawapaswi kuwa wasingiziaji, wala wasikuwe watumwa wa pombe, lakini wakuwe wenye kutoa mafundisho mazuri.


Kwa ajili ya maumivu ya tumbo lako na uzaifu wa mwili wako wa kila mara, tangu sasa usikunywe maji tu, lakini utumie divai kidogo.


Hapaswi kuwa mulevi wala mupiganaji, lakini akuwe mupole mwenye kupenda amani, wala asikuwe mutu wa kupenda feza.


Munapoingia ndani ya hema la mukutano, wewe na wana wako musikunywe divai wala kileo chochote, kama sivyo mutakufa. Hili litakuwa sharti ambalo vizazi vyenu vyote wanapaswa kulifuata siku zote.


Ndani ya kinywa kimoja munatoka maneno ya sifa na ya laana. Wandugu zangu, mambo haya hayapaswi kuwa vile.


Kwa maana musimamizi wa kanisa anapaswa kuwa mutu asiyeshitakiwa neno, kwa sababu yeye ni mwangalizi wa kazi ya Mungu. Hapaswi kuwa mutu mwenye kiburi, wala mukali, mulevi, mugomvi wala mwenye kutafuta mali kwa njia mbaya.


Inafaa wasaidizi wa kanisa wakuwe kila mutu na muke mumoja tu, na wanapaswa kuwa watu wenye kuongoza vizuri watoto wao pamoja na jamaa zao.


Kuhani yeyote asikunywe divai anapoingia katika kiwanja cha ndani.


Unisaidie, ee Yawe! Watu wema wamekwisha; waaminifu wametoweka kati ya watu.


Ee Yawe, katika haki yako, uisawanishe njia yako mbele yangu. Uniongoze kwa sababu ya waadui zangu.


Ninawaonya, muchunge lile kundi Mungu alilowapatia, si kwa kulazimishwa, lakini kwa mapenzi yenu sawa vile Mungu anavyotaka. Musitumike kwa ajili ya tamaa mbaya ya mali, lakini kwa kujitoa kwa moyo mwema.


Vinywa vyao ni kama kaburi wazi, ndimi zao ni za kudanganya, ndani ya midomo yao munatoka sumu kali sawa ya nyoka.


Uko tayari siku zote kusema mabaya; kazi ya ulimi wako ni kutunga uongo.


Basi musimamizi wa kanisa anapaswa kuwa mutu asiyeshitakiwa neno lolote. Sherti akuwe na muke mumoja tu, akuwe mukadirifu, mwenye akili, akuwe mwema na mwenye kupenda kukaribisha wageni na mwenye kujua kufundisha.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite