Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Timoteo 3:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Yeye hapaswi kuwa mwamini mupya; kusudi asitawaliwe na kiburi na kuhukumiwa kama vile Shetani alivyokuwa.

Gade chapit la Kopi




1 Timoteo 3:6
24 Referans Kwoze  

yeye anajaa majivuno wala hajui kitu. Yeye yuko na ulema wa kubishana na kugombezana juu ya maana ya maneno. Na hayo yanaleta wivu, makelele, matukano, masingiziano


Na hivi vilevile, ninyi vijana, munapaswa kuwatii hao wazee. Ninyi wote munapaswa kuwa na unyenyekevu, mupate kutumikiana; maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Mungu anawapinga wenye kiburi, lakini anawajalia wanyenyekevu neema.”


Kama vile watoto wachanga wanaotamani maziwa, na ninyi vilevile mukuwe na hamu ya kunywa maziwa safi ya kiroho, kusudi mupate kukomaa na kuokolewa.


Lakini, kusudi nisijivune kupita kipimo kwa ajili ya kupokea ufunuo wa ajabu, nilitiwa katika mwili wangu kitu kinachoniumiza kama mwiba. Kitu kile ni kama mujumbe wa Shetani kwa kunipiga na kunizuiza nisijivune kupita kipimo.


Sasa tuangalie mambo yanayoelekea nyama zinazotolewa kwa kutambikia sanamu za miungu: tunajua kwamba “sisi wote tuko na elimu,” kama vile munavyozoea kusema. Elimu inamufanya mutu kuwa na kiburi, lakini upendo unawajenga watu katika imani.


Kweli wandugu zangu, sikuweza kusema nanyi kama watu wanaotawaliwa na Roho wa Mungu, lakini kama watu wanaotawaliwa na mambo ya kidunia. Mungali kama watoto wachanga katika mambo ya Kikristo.


Kweli, siku ya Yawe wa majeshi inakuja juu ya wote wenye kiburi na majivuno, juu ya wote wanaojitukuza,


Kiburi cha mutu kinamuzaraulisha mwenyewe, lakini munyenyekevu wa roho atapata heshima.


Majivuno ya ndani ya moyo yanaleta maangamizi, lakini unyenyekevu unaleta heshima.


Lakini Hezekia hakumutolea Yawe shukrani kwa yale yote aliyomutendea kwa sababu moyo wake ulikuwa umejaa majivuno. Hii ikasababisha kutaabika kwa inchi ya Yuda na Yerusalema.


Lakini wakati mufalme Uzia alipokuwa na nguvu, moyo wake akajaa kiburi ambacho kilisababisha maangamizi yake. Akamwasi Yawe wake kwa kuingia ndani ya hekalu akikusudia kufukiza ubani juu ya mazabahu.


Sasa, wewe Amazia umewashinda kabisa Waedomu, na moyo wako unakufanya ujivune. Ufurahie utukufu wako, ukae katika nyumba yako; kwa nini kujitafutia taabu zitakazokuangamiza wewe mwenyewe pamoja na watu wako wa Yuda?”


bila kujitukuza mwenyewe juu ya wandugu zake, wala kuiweka kando amri hii kwa namna yoyote, kusudi aweze kudumu katika utawala, yeye na wazao wake katika Israeli.


musikuwe na kiburi na kumusahau Yawe, Mungu wenu, aliyewatoa katika inchi ya Misri, pahali mulipokuwa watumwa.


Mukumbuke vilevile wamalaika wale waliokosa kulinda vema cheo chao, lakini wakaacha makao yao: Mungu akawaweka katika nafasi ya giza, wakifungwa minyororo ya milele kwa kungojea Siku ile ya hukumu.


Kwa maana Mungu hakuwahurumia wale wamalaika waliofanya zambi, lakini aliwatupa katika jehenamu. Wao wanalindwa mule wakifungwa minyororo katika giza nzito wakingojea Siku ile ya hukumu.


Watakuwa wenye kutoana, wenye kichwa kigumu, wenye majivuno na wenye kupenda tamaa ya vitu kuliko kumupenda Mungu.


Naye Yesu akamwambia: “Nilimwona Shetani akianguka kama umeme toka mbinguni.


Vilevile inafaa akuwe mutu mwenye kushuhudiwa vizuri na watu wa inje ya kanisa, kusudi asizarauliwe na kunaswa katika mutego wa Shetani.


Kisha kulishinda vibaya kundi la waasakri wa kaskazini na kuua maelfu, ataanza kujisifu, lakini hataendelea kuwa mushindi.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite