Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Timoteo 3:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Basi musimamizi wa kanisa anapaswa kuwa mutu asiyeshitakiwa neno lolote. Sherti akuwe na muke mumoja tu, akuwe mukadirifu, mwenye akili, akuwe mwema na mwenye kupenda kukaribisha wageni na mwenye kujua kufundisha.

Gade chapit la Kopi




1 Timoteo 3:2
20 Referans Kwoze  

Basi, mutumishi wa Bwana hapaswi kugombana. Anapaswa kuwa mupole kwa watu wote, anayejua kufundisha na muvumilivu.


Muwasaidie watu wa Mungu katika mahitaji yao na muwakaribishe wageni.


Usimwandike katika hesabu ya wajane mujane yeyote ambaye hajatimiza umri wa miaka makumi sita. Tena inafaa akuwe yule aliyeolewa na mume mumoja tu.


Mukaribishane ninyi kwa ninyi pasipo kunungunika.


Mukuwe waangalifu na mukeshe, kwa maana adui yenu Shetani anazungukazunguka kama simba anayenguruma akitafuta yule atakayerarua.


Musisahau kuwakaribisha wageni, maana kwa kufanya hivi wamoja wamewakaribisha wamalaika pasipo kujua.


Uwaambie wazee wanaume wakuwe wakadirifu, wenye heshima na utaratibu, wenye kukamilika katika imani, katika upendo na uvumilivu.


kusudi mupate kuwa bila kosa na kuwa na maisha safi. Hivi mutakuwa watoto wakamilifu wa Mungu wasiokuwa na kilema kati ya watu waovu na wapotovu wa dunia hii. Munapaswa kuangaza kati ya watu hawa kama vile nyota zinavyoangaza katika mbingu,


Mwisho wa vitu vyote unakaribia kutimia. Kwa hiyo mukuwe wenye akili na waangalifu, kusudi mukuwe na uwezo wa kuomba.


Kwa maana sisi wote tunaishi katika ushirika na Kristo ikiwa tunachunga mpaka mwisho lile tumaini tulilopata kwa mwanzo.


Wao wanafundisha kwamba ni vibaya kuoana, na wanawakataza watu kula vyakula fulani fulani. Lakini Mungu aliumba vyakula vile kusudi watu waliokwisha kumwamini na kutambua ukweli wapate kuvitumia wakisha kumushukuru.


Wote wawili walikuwa wenye haki mbele ya Mungu, walishika kwa ukamilifu amri na maagizo yote ya Bwana.


Maana walinzi wa Israeli wote ni vipofu; wote hawana akili yoyote. Wote ni kama imbwa bubu wasioweza kufoka, wanalala tu na kuota ndoto, wanapenda sana kusinzia!


Kulikuwa vilevile nabii mumoja mwanamuke, aliyeitwa Ana, aliyekuwa binti ya Fanueli, wa kabila la Aseri. Yeye alikuwa muzee sana. Aliishi miaka saba na mume wake tangu alipoolewa.


Vilevile wasaidizi wanaotumika katika kanisa wanapaswa kuwa watu wenye heshima. Hawapaswi kuwa wenye nia mbili katika masemi yao wala wenye kunywa pombe kwa uwingi wala wenye kutafuta mali kwa njia isiyokuwa sawa;


Inafaa wasaidizi wa kanisa wakuwe kila mutu na muke mumoja tu, na wanapaswa kuwa watu wenye kuongoza vizuri watoto wao pamoja na jamaa zao.


Sherti ajulikane kwa matendo yake mema. Anapaswa kuwa mutu aliyeadibisha watoto wake vizuri, aliyekaribisha wageni, aliyewapokea watu wa Mungu akiwanawisha miguu, aliyewasaidia wenye taabu na aliyejitolea kwa kutenda mema ya kila namna.


Usiweke mikono juu ya mutu kwa haraka, wala usishiriki zambi za watu wengine. Ujilinde wewe mwenyewe katika maisha safi.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite