Basi musimamizi wa kanisa anapaswa kuwa mutu asiyeshitakiwa neno lolote. Sherti akuwe na muke mumoja tu, akuwe mukadirifu, mwenye akili, akuwe mwema na mwenye kupenda kukaribisha wageni na mwenye kujua kufundisha.
Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo na kwa ndugu yetu Timoteo, sisi watumishi wa Yesu Kristo. Tunawaandikia watu wote wa Mungu wanaoungana na Yesu Kristo, wanaoishi Filipi, pamoja na wazee wa kanisa na wasaidizi.
Vilevile wasaidizi wanaotumika katika kanisa wanapaswa kuwa watu wenye heshima. Hawapaswi kuwa wenye nia mbili katika masemi yao wala wenye kunywa pombe kwa uwingi wala wenye kutafuta mali kwa njia isiyokuwa sawa;