Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Timoteo 3:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Neno hili ni la kweli; kama mutu anatamani kazi ya musimamizi wa kanisa anatamani kazi nzuri.

Gade chapit la Kopi




1 Timoteo 3:1
19 Referans Kwoze  

Kwa maana musimamizi wa kanisa anapaswa kuwa mutu asiyeshitakiwa neno, kwa sababu yeye ni mwangalizi wa kazi ya Mungu. Hapaswi kuwa mutu mwenye kiburi, wala mukali, mulevi, mugomvi wala mwenye kutafuta mali kwa njia mbaya.


Mujichunge ninyi wenyewe na muchunge vilevile lile kundi lote Roho Mutakatifu alilowapatia kusudi mukuwe wasimamizi wao. Hivi mutaweza kuchunga kanisa la Mungu ambalo alijipatia kwa damu ya Mwana wake.


Ninawaonya, muchunge lile kundi Mungu alilowapatia, si kwa kulazimishwa, lakini kwa mapenzi yenu sawa vile Mungu anavyotaka. Musitumike kwa ajili ya tamaa mbaya ya mali, lakini kwa kujitoa kwa moyo mwema.


Neno hili ni la kuaminiwa nalo linastahili kukubaliwa kabisa: Kristo Yesu alikuja katika dunia kwa kuokoa wenye zambi. Na mimi ni wa kwanza mwenye zambi kati yao,


Kwa maana mulikuwa kama kondoo wanaopotea, lakini sasa mumerudi kwa yule anayekuwa muchungaji na mwangalizi wa roho zenu.


Muangalie vizuri, kusudi hata mutu mumoja asijikoseshe mwenyewe kupata neema ya Mungu, wala asikuwe sawa shina la mumea unaotoa matunda machungu na kuleta fujo kati yenu na kuambukiza watu wengi.


Maneno haya ni ya kuaminiwa: Kama tumekufa pamoja naye, tutaishi pamoja naye vilevile.


Neno hilo ni la kuaminiwa, nalo linastahili kukubaliwa kabisa.


Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo na kwa ndugu yetu Timoteo, sisi watumishi wa Yesu Kristo. Tunawaandikia watu wote wa Mungu wanaoungana na Yesu Kristo, wanaoishi Filipi, pamoja na wazee wa kanisa na wasaidizi.


Vilevile ninawaambia, ndivyo wamalaika wa Mungu wanavyofurahi kwa ajili ya mwenye zambi mumoja anayegeuka toka zambi zake.”


Neno hilo ni la kuaminiwa. Ninataka uyatilie maneno hayo mukazo, kusudi watu walioamini Mungu wajitolee kwa kuzidi kutenda mema. Jambo hilo ni zuri na lenye mafaa kwa watu.


Yeye amefanya vile kwa kuwatayarisha watu wa Mungu kwa kazi ya utumishi kusudi mwili wa Kristo upate kujengwa.


“Kwa sababu imeandikwa hivi katika kitabu cha Zaburi: ‘Makao yake yabakie ukiwa na mutu asiishi ndani yake.’ Na imeandikwa tena: ‘Mutu mwingine atwae kazi yake.’


Kati yenu kusikuwe hata mutu mumoja anayeteswa kwa sababu yeye ni mwuaji, mwizi, mutenda mabaya au mwenye kujiingiza katika mambo ya watu wengine.


Tunawasihi wandugu, muwaonye wale wanaokuwa wavivu, muwatie moyo wale wanaoregea, muwasaidie wale wanaokuwa zaifu, na mukuwe wavumilivu kwa watu wote.


Sasa ninasema na ninyi watu wa mataifa mengine. Nami ninafurahia kazi yangu, kwa kuona nimetumwa kuwa muhubiri wa watu wa mataifa.


Tunda la mwenye haki ni muti wa uzima, na mwenye hekima anavuta watu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite