Neno hilo ni la kuaminiwa. Ninataka uyatilie maneno hayo mukazo, kusudi watu walioamini Mungu wajitolee kwa kuzidi kutenda mema. Jambo hilo ni zuri na lenye mafaa kwa watu.
Vilevile, ninyi waume, mukae na wake wenu mukifahamu kwamba wao ni kiumbe kizaifu. Munapaswa vilevile kuwapa heshima kwa sababu watapokea pamoja nanyi zawadi ya uzima. Mufanye hivi kusudi maombi yenu yasizuizwe.
Lakini muda ule ulipotimia tukaondoka na kuendelea na safari yetu. Waamini wote pamoja na wanawake na watoto wao wakatusindikiza mpaka mbali na hata kufika kwenye kivuko cha muji. Kule sisi wote tukapiga magoti na kuomba.
Kornelio akamukazia macho akiwa ameshikwa na woga, akamwuliza: “Bwana, ni nini?” Malaika akamujibu: “Mungu amesikia maombi yako na kupendezwa na misaada unayotoa kwa wamasikini, na kwa hiyo anakukumbuka.
Yeye alikuwa mwenye kuogopa Mungu, naye alimwabudu Mungu pamoja na watu wote waliokuwa kwake. Aliwasaidia wamasikini wengi, naye alikuwa akimwomba Mungu siku zote.
Yesu akawajibu: “Kweli ninawaambia: mukimwamini Mungu pasipo kuwa na shaka, hamutaweza kufanya tu kama nilivyotendea muti huu, lakini vilevile mutaweza kuuambia mulima huu: ‘Ondoka hapa, ujitupe katika bahari,’ na itakuwa vile.
naye akamwambia: “Kwa sababu umetoa ombi hili, na haukujiombea maisha marefu au mali, na wala haukuomba waadui zako waangamizwe, lakini umejiombea hekima ya kutoa hukumu au kutenda haki,
Tunawaandikia ninyi kanisa la Mungu linalokuwa Korinto, ninyi ambao mumetakaswa kwa njia ya kuungana kwenu na Yesu Kristo na mumeitwa na Mungu kuwa watu wake. Vilevile barua hii ni kwa wote wanaoabudu jina la Bwana Yesu Kristo fasi zote, anayekuwa Bwana wao na Bwana wetu vilevile.
Lakini Mungu ashukuriwe, maana yeye ndiye anayetupatia ushindi siku zote katika ushirika wetu pamoja na Kristo. Anatutumia sisi kwa kutambulisha Kristo pahali pote kama vile harufu nzuri ya marasi inavyosambaa popote.
Kwa maana tokea kwenu neno la Bwana lilienea, si katika Makedonia na Akaya tu, lakini habari za imani kwa Mungu zilisambaa fasi zote, hata sisi hatukukuwa tena na lazima ya kusema neno juu ya ile.