Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Timoteo 2:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Basi, ninataka watu waombe Mungu wakiinua mikono juu, ikiwa imetakaswa, nao wafanye vile bila kasirani wala ubishi.

Gade chapit la Kopi




1 Timoteo 2:8
48 Referans Kwoze  

Muinue mikono kuelekea pahali patakatifu, na kumutukuza Yawe!


Wema wako ni bora kuliko maisha. Nitakusifu kwa midomo yangu.


Basi tumwendee Mungu kwa moyo wa uaminifu, kwa imani kamilifu, kwa moyo uliosafishwa toka zamiri mbaya na mwili uliosafishwa na maji safi.


Neno hilo ni la kuaminiwa. Ninataka uyatilie maneno hayo mukazo, kusudi watu walioamini Mungu wajitolee kwa kuzidi kutenda mema. Jambo hilo ni zuri na lenye mafaa kwa watu.


Mumukaribie Mungu, naye atawakaribia. Musafishe mikono yenu, ninyi wenye zambi! Mutakase mioyo yenu, ninyi wenye nia mbili!


Kisha Yesu akatoka nao katika muji na kwenda karibu na kijiji cha Betania na pale akainua mikono yake juu na kuwabariki.


Munapoinua mikono yenu kwa kuomba, nitauficha uso wangu nisiwaone. Hata mukiomba sana sitawasikia, maana mikono yenu imejaa damu.


Vilevile, ninyi waume, mukae na wake wenu mukifahamu kwamba wao ni kiumbe kizaifu. Munapaswa vilevile kuwapa heshima kwa sababu watapokea pamoja nanyi zawadi ya uzima. Mufanye hivi kusudi maombi yenu yasizuizwe.


Kwa sababu hiyo, ninataka wajane wanaokuwa wangali vijana waolewe, wazae watoto na kutunza nyumba zao, kusudi waadui wasipate nafasi ya kutuchongea.


Lakini muda ule ulipotimia tukaondoka na kuendelea na safari yetu. Waamini wote pamoja na wanawake na watoto wao wakatusindikiza mpaka mbali na hata kufika kwenye kivuko cha muji. Kule sisi wote tukapiga magoti na kuomba.


Kornelio akamukazia macho akiwa ameshikwa na woga, akamwuliza: “Bwana, ni nini?” Malaika akamujibu: “Mungu amesikia maombi yako na kupendezwa na misaada unayotoa kwa wamasikini, na kwa hiyo anakukumbuka.


Yeye alikuwa mwenye kuogopa Mungu, naye alimwabudu Mungu pamoja na watu wote waliokuwa kwake. Aliwasaidia wamasikini wengi, naye alikuwa akimwomba Mungu siku zote.


Kisha akapiga magoti, akalalamika, akisema: “Bwana, usiwahesabie zambi hii.” Na nyuma ya kusema maneno haya, akakufa.


Hakika, ningetamani watu wote wakuwe kama mimi, lakini kila mutu amepewa zawadi yake ya kipekee na Mungu, mumoja zawadi hii, na mwingine zawadi ile.


Naye akaniambia: ‘Kornelio, Mungu amesikia maombi yako na kukukumbuka kwa ajili ya misaada unayotoa kwa wamasikini.


Yesu akamwambia: “Ee mama, unisadiki; kutakuwa wakati hamutamwabudu Baba juu ya mulima huu wala Yerusalema.


Halafu Yesu akasema: “Baba uwasamehe, kwa maana hawajui jambo wanalofanya.” Waaskari wakagawanya nguo zake kwa kuzipigia kura.


Yesu akawajibu: “Kweli ninawaambia: mukimwamini Mungu pasipo kuwa na shaka, hamutaweza kufanya tu kama nilivyotendea muti huu, lakini vilevile mutaweza kuuambia mulima huu: ‘Ondoka hapa, ujitupe katika bahari,’ na itakuwa vile.


Lakini mimi ninawaambia: muwapende waadui zenu na muwaombee wale wanaowatesa.


Kama ningalikusudia maovu ndani ya moyo, Yawe hangalinisikiliza.


Ninanawa mikono yangu kuonyesha kama sina kosa, na kuizunguka mazabahu yako, ee Yawe,


Ni mutu wa matendo mema na moyo safi, asiyefuata mambo ya ovyo, wala kuapa kwa uongo.


ingawa sijatesa watu kwa mukono wangu, na maombi yangu kwa Mungu ni safi.


Utusamehe makosa yetu, kama sisi tunavyowasamehe wanaotukosea,


Sadaka ya mwovu ni kitu cha kuchukiza sana. Inachukiza zaidi akiitoa kwa nia mbaya.


Sadaka ya waovu ni chukizo kwa Yawe, lakini maombi ya watu wa usawa yanamufurahisha Mungu.


Lakini wao walipokuwa wagonjwa, mimi nilivaa magunia kuonyesha huzuni, nilijitesa kwa kufunga kula chakula. Niliomba nikikuwa nimeinamisha kichwa.


naye akamwambia: “Kwa sababu umetoa ombi hili, na haukujiombea maisha marefu au mali, na wala haukuomba waadui zako waangamizwe, lakini umejiombea hekima ya kutoa hukumu au kutenda haki,


Sikiliza sauti ya ombi langu, ninapokulilia unisaidie, ninapoinua mikono yangu kuelekea hekalu lako takatifu.


Upokee maombi yangu kama ubani; ninapoinua mikono yangu kwako, unikubali kama sadaka ya magaribi.


Tunawaandikia ninyi kanisa la Mungu linalokuwa Korinto, ninyi ambao mumetakaswa kwa njia ya kuungana kwenu na Yesu Kristo na mumeitwa na Mungu kuwa watu wake. Vilevile barua hii ni kwa wote wanaoabudu jina la Bwana Yesu Kristo fasi zote, anayekuwa Bwana wao na Bwana wetu vilevile.


Lakini Mungu ashukuriwe, maana yeye ndiye anayetupatia ushindi siku zote katika ushirika wetu pamoja na Kristo. Anatutumia sisi kwa kutambulisha Kristo pahali pote kama vile harufu nzuri ya marasi inavyosambaa popote.


Wandugu zangu, ninataka mujue kwamba mambo yaliyonifikia yamesaidia kwa kuendelesha Habari Njema.


Kwa maana tokea kwenu neno la Bwana lilienea, si katika Makedonia na Akaya tu, lakini habari za imani kwa Mungu zilisambaa fasi zote, hata sisi hatukukuwa tena na lazima ya kusema neno juu ya ile.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite