Mukuwe na mwenendo muzuri kati ya wapagani, kusudi wakiwasingizia kwamba mumefanya mabaya, wapate kuona matendo yenu mema na wamutukuze Mungu siku ile ya kuja kwake.
Katika muji wa Yopa kulikuwa mwanafunzi mumoja mwanamuke aliyeitwa Tabita. (Katika kigriki ni “Dorika,” maana yake “Pongo”.) Mwanamuke huyu alikuwa akifanya matendo mengi mema na kuwasaidia wamasikini.
Neno hilo ni la kuaminiwa. Ninataka uyatilie maneno hayo mukazo, kusudi watu walioamini Mungu wajitolee kwa kuzidi kutenda mema. Jambo hilo ni zuri na lenye mafaa kwa watu.
Kwa maana sisi ni viumbe vya Mungu, na kwa kuungana kwetu na Yesu Kristo, alituumba kusudi tuishi maisha ya matendo mema, ambayo Mungu alitutayarishia tangu mbele tupate kuyatenda.
Yeye alijitoa mwenyewe kwa ajili yetu, kusudi atukomboe toka uovu wote na kututakasa tupate kuwa watu wake wa pekee, watu wanaokuwa na hamu ya kufanya kazi nzuri.
Mara moja Petro akaenda pamoja nao. Naye alipofika wakamupeleka ndani ya chumba cha gorofi. Wajane wote wakamuzunguka Petro, wakilia na kumwonyesha kanzu na nguo zote Dorika alizowashonea wakati alipokuwa angali muzima.
Ninataka vilevile wanawake wavae kwa namna inayostahili. Inafaa wajipambe kwa adabu na kwa ukadirifu, si kwa namna mbalimbali za urembo za kusuka nywele, wala kwa zahabu, wala kwa ushanga au nguo za bei kali.