Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Timoteo 2:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Mbele ya yote, ninawaonya ninyi kuwaombea watu wote. Muombe Mungu awasaidie na kuwabariki, na mumushukuru kwa ajili yao.

Gade chapit la Kopi




1 Timoteo 2:1
26 Referans Kwoze  

Wandugu, tunapaswa kumushukuru Mungu siku zote kwa ajili yenu. Inatufaa kufanya vile kwa maana imani yenu inaongezeka, nao upendo wenu ninyi kwa ninyi unazidi kuongezeka.


Basi muitikiane zambi ninyi kwa ninyi na kuombeana kusudi mupate kuponyeshwa. Maombi ya bidii ya mwenye haki ni yenye faida kubwa.


Mumushukuru Mungu Baba siku zote kwa kila jambo, kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo.


Basi, mutumishi wa Bwana hapaswi kugombana. Anapaswa kuwa mupole kwa watu wote, anayejua kufundisha na muvumilivu.


anayetaka watu wote waokolewe na kuweza kutambua ukweli.


Ninamushukuru Mungu wangu kwa ajili yenu kila mara ninapowakumbuka.


Lakini tunatamani sana kwamba kila mumoja kati yenu aendelee kuonyesha bidii ile mpaka mwisho, kusudi mambo yale munayotumainia yapate kutimizwa.


Uwaambie wasiseme mabaya juu ya mutu, lakini wakuwe wenye kupenda amani na wema, na wenye kuonyesha upole mbele ya kila mutu.


Kwa maana neema ya Mungu inayoleta wokovu kwa watu wote imeonekana waziwazi.


Mujane wa kweli asiyekuwa na mutu yeyote wa kumusaidia, anamutumainia Mungu, na kudumu kumutolea mahitaji yake na kumwomba muchana na usiku.


Kwanza nimewatolea mafundisho haya ambayo mimi mwenyewe nilipokea: Kristo alikufa kwa sababu ya zambi zetu kama vile Maandiko Matakatifu yanavyosema.


Mungu hahesabu tena nyakati zile watu walipokuwa katika ujinga, lakini sasa anatangaza kwa watu wote, na nafasi zote kwamba wageuke toka zambi zao.


Na Bwana awaongezee na kuwazidishia upendo munaokuwa nao ninyi kwa ninyi na kwa watu wote, kama vile sisi nasi tunavyowapenda ninyi.


Lakini asante kwa Mungu, kwa maana ninyi muliokuwa zamani watumwa wa zambi mumetii sasa kwa moyo wenu wote kanuni za mafundisho muliyopewa.


Kwanza ninamushukuru Mungu wangu kwa njia ya Yesu Kristo kwa ajili yenu ninyi wote, kwa sababu habari za imani yenu zinasambaa katika dunia nzima.


Jina lake tukufu litukuzwe milele; utukufu wake ujae katika ulimwengu wote! Amina, Amina!


Ni kwa hiyo tulimusihi Tito atimize kazi hiyo ya kuwaongoza ninyi kuwa na moyo wa kutoa sawa alivyoianzisha.


Basi ninawaomba musiregee kwa sababu ya mateso ninayopata kwa ajili yenu, kwa maana yanawaletea utukufu.


Haya yote yatatendeka kusudi waweze kumutolea Mungu wa mbinguni sadaka zinazomupendeza na waombee maisha yangu mimi mufalme na watoto wangu.


Mushugulike na kuleta ustawi katika muji ule ambamo nimewahamishia. Muuombee muji huo kwa Yawe, maana ukistawi ninyi vilevile mutastawi.


Mumwombe Mungu kila wakati mukiongozwa na Roho. Mumwombe na kumusihi kwa kila namna. Kwa hiyo mukeshe bila kuchoka mukiwaombea watu wote wa Mungu.


Musijisumbue juu ya neno lolote, lakini katika kila neno mutoe mahitaji yenu kwa Mungu, mukimwomba, mukimusihi na kumushukuru.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite