Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Timoteo 1:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Ninamushukuru Bwana wetu Kristo Yesu aliyenitia nguvu, kwa sababu alinihesabu kuwa mwaminifu hata akaniweka kwa kazi yake.

Gade chapit la Kopi




1 Timoteo 1:12
26 Referans Kwoze  

Ninaweza vyote kwa njia ya Kristo anayenitia nguvu.


Lakini Bwana alinisaidia, akanitia nguvu nipate kuitangaza Habari Njema kwa ukamilifu kusudi watu wa mataifa mengine wapate kuisikia. Nami nikaokolewa toka katika kinywa cha simba.


Mimi nimekuwa mutumishi wa kanisa kufuatana na kazi ile Mungu aliyonipa kwa ajili yenu. Kazi yenyewe ni kutangaza Neno lake kwa ukamilifu.


na kila mutu akubali kwamba Yesu ni Bwana, naye Mungu Baba atatukuzwa kwa njia hiyo.


Kwa wema wake, Mungu ametupatia utumishi huu, na kwa sababu hii sisi hatukati tumaini.


Kuelekea wale ambao hawajaoa wala kuolewa, sina neno la kuwaamuru kutoka kwa Bwana. Lakini nitawatolea shauri kufuatana na vile ninavyokuwa mutu anayestahili kuaminiwa, kutokana na neema niliyopewa na Bwana.


Lakini Saulo akazidi kuhubiri na uwezo, akawashinda Wayuda waliokaa Damasiki akihakikisha wazi kwao kwamba Yesu ndiye Kristo.


Lakini Bwana akamwambia: “Kwenda tu, kwa maana nimemuchagua mutu huyu kwa kunitumikia, kusudi atangaze jina langu kwa mataifa, kwa wafalme na kwa Waisraeli.


Kisha yeye na watu wa nyumba yake wakabatizwa. Naye akatusihi akisema: “Ikiwa munakubali kweli kwamba ninamwamini Bwana, basi mufike mupange ndani ya nyumba yangu.” Akatulazimisha tuitike.


Mafundisho haya yanalingana na Habari Njema ya utukufu wa Mungu mwenye baraka, ambayo nilipewa nipate kuihuburi.


Lakini kwa neema ya Mungu nimekuwa sawa hivi ninavyokuwa, na neema yake niliyopewa haikukuwa ya bure, lakini nilitumika zaidi sana kuliko mitume wote wengine. Hakika si mimi, lakini ni neema ya Mungu inayokuwa pamoja nami.


kusudi watu wote wamuheshimu Mwana kama vile wanavyomuheshimu Baba. Asiyemuheshimu Mwana, hamuheshimu Baba aliyemutuma.


Basi, Apolo ni nani? Na Paulo ni nani? Sisi ni watumishi wa Mungu, waliowaonyesha ninyi njia ya kuamini. Tumefanya vile kila mumoja wetu kwa kadiri ya zawadi aliyopewa na Bwana.


Kwa maana ninyi wote mumekuwa wana wa Mungu kwa njia ya imani na kuungana na Yesu Kristo.


Kwa hiyo hakuna tena umbalimbali kati ya Wayuda na watu wa mataifa mengine, kati ya watumwa na watu huru, mwanaume na mwanamuke; kwa maana ninyi wote ni mumoja katika kuungana kwenu na Yesu Kristo.


Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo, niliyeitwa kuwa mutume wa Kristo Yesu kwa amri ya Mungu Mwokozi wetu na ya Kristo Yesu tunayemutumainia.


Ninakuandikia wewe Timoteo mwana wangu wa kweli katika imani. Ninakutakia neema na rehema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na kwa Kristo Yesu Bwana wetu.


Mbele ya Mungu anayevipatia vitu vyote uzima, na mbele ya Kristo Yesu aliyetoa ushuhuda wa kweli mbele ya Pontio Pilato, ninakuagiza maneno haya:


Wewe umesikia mafundisho niliyotoa mbele ya washuhuda wengi. Nawe sasa uyafundishe kwa watu waaminifu watakaoweza vilevile kuyatoa kwa watu wengine.


Ninakutumia barua hii, wewe Tito, mwana wangu wa kweli katika imani tunayoshiriki pamoja. Ninakutakia neema na amani kutoka kwa Mungu Baba na kwa Yesu Kristo Mwokozi wetu.


lakini kwa ajili ya upendo, ninapendelea kukusihi, mimi Paulo ninayekuwa muzee, na zaidi sasa ninakuwa mufungwa kwa ajili ya Yesu Kristo.


Akawaambia: ‘Ninyi vilevile muende kutumika katika shamba langu la mizabibu, nami nitawalipa sawa na haki yenu.’


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite