Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Timoteo 1:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Sheria imewekwa kwa ajili ya waasherati, wanaume wanaozini wao kwa wao, wenye kuuzisha watu, wasema uongo, wale wanaofanya viapo vya uongo na kwa ajili ya wote wanaofanya matendo yanayokuwa umbalimbali na mafundisho ya kweli.

Gade chapit la Kopi




1 Timoteo 1:10
34 Referans Kwoze  

Usilale na mwanaume mwenzako kama vile ni mwanamuke. Hilo ni chukizo.


Maana kutakuja wakati watu watakapokataa kusikiliza mafundisho ya kweli, lakini watafuata tamaa zao wenyewe wakijitafutia walimu wengi kwa kuwafundisha mambo yale wanayotamani kusikia.


Kwa hiyo Mungu aliwaacha wafuate tamaa zao za haya. Wanawake wao wanabadilisha matumizi ya kawaida na matumizi isiyokuwa ya kawaida.


Hakuna kitu chochote kichafu kitakachoingia ndani yake, wala yeye anayefanya machukizo na kusema uongo; lakini wale tu ambao majina yao yaliandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo.


Kama mutu akifundisha mafundisho mengine, naye hakubali maneno ya kweli ya Bwana wetu Yesu Kristo wala mafundisho yanayolingana na dini yetu,


Mukumbuke vilevile watu wa Sodoma na Gomora na wa miji iliyokuwa kandokando wanaokuwa sawasawa na wamalaika hawa. Walifanya uasherati na mambo ya kimwili yasiyokuwa ya kawaida ya asili. Watu hawa wanapokea hukumu ya moto wa milele kuwa mufano wazi kwa watu wote.


Anapaswa kushika Neno la kweli linalolingana na mafundisho yetu. Hivi ataweza kuwaonya watu kwa njia ya mafundisho ya kweli na kuwashinda wale wanaomupinga.


Lakini watu wenye woga, wasioamini, wenye machukizo, wauaji, wazinzi, wachawi, wanaoabudu sanamu na wote wanaosema uongo, fungu lao ni katika lile ziwa la moto na ndani ya mawe ya kiberiti yanayowaka moto. Hiki ndicho kifo cha pili.”


Ndoa inapaswa kuheshimiwa na watu wote, mume na muke wake wanapaswa kujikinga na uchafu, kwa sababu Mungu atawahukumu wazinzi na waasherati.


Kama mwanaume yeyote akilala na mwanaume mwenzake sawa vile ni mwanamuke, basi, wote wawili wanapaswa kuuawa maana wamefanya jambo linalokuwa chukizo na damu yao itakuwa juu yao wenyewe.


Lakini mbali ya muji ule kuna watu wenye kuchukiza, wachawi, wazinzi, wauaji, wanaobudu sanamu na wasema uongo na wote wanaoupenda.


Ushike maneno ya kweli niliyokufundisha, yapate kuwa mufano kwako. Ushikamane na imani na upendo unaokuwa nao kwa njia ya kuungana kwako na Kristo Yesu.


Baba yenu ni Shetani, nanyi munataka kutimiza sawa vile huyo baba yenu anavyotamani. Yeye ni mwuaji siku zote, naye hajasimama katika ukweli, kwa sababu ndani yake hakuna ukweli. Wakati anaposema uongo, masemi yake yanatokana na tabia yake, kwa sababu yeye ni mwongo na baba ya uongo.


Anayemukamata mutu kwa kinguvu kusudi amwuzishe au kumufanya mutumwa wake, hakika atauawa.


Wakamwita Loti na kumwuliza: “Wako wapi wale wanaume waliokuja kwako? Uwatoshe inje. Tunataka kulala nao.”


Ushuhuda huo ni wa kweli. Basi kwa hiyo uwaonye vikali, kusudi wapate kuwa na imani kamili.


Usitaje bure jina langu mimi Yawe, Mungu wako, maana mimi Yawe sitaacha kumwazibu yeyote anayetaja bure jina langu.


mudalasini, vitu vyote vya kufukiza, marasi, ubani, divai, mafuta, unga nzuri, ngano, ngombe, kondoo, farasi, magari, watumwa na hata roho za watu.


Mutu yeyote asikusudie kumutendea mwenzake ubaya wala musiape uongo, maana ninayachukia sana matendo hayo. Ni mimi Yawe ninayesema hivyo.


Wanachosema ni maneno matupu; wanaapa na kufanya mapatano ya bure; haki imekuwa si haki tena, inachipuka kama mimea yenye sumu katika shamba.


“Mutu yeyote akimwiba Mwisraeli mwenzake na kumufanya kuwa mutumwa wake au kumwuzisha katika utumwa, mutu huyo anapaswa kuuawa. Ndivyo mutakavyokomesha uovu kati yenu.


Yawe wa majeshi anasema: Kisha nitawakaribia kwa kuwahukumu. Sitasita kutoa ushuhuda juu ya wachawi, wazinzi, watoa ushuhuda wa uongo, wanaopunja mushahara wa watumishi, wanaowatesa wajane na wayatima, wanaozuia mugeni asipate haki yake na wale wasioniogopa mimi.


Yawe wa majeshi anasema kwamba yeye mwenyewe ataipeleka laana hiyo. Itapenya kila nyumba ya mwizi na kila nyumba ya mwenye kuapa uongo kwa kutumia jina lake; itakaa mule na kuteketeza nyumba hiyo yote, mbao na mawe.


Maana mimi nilitoroshwa kutoka inchi ya Waebrania na hapa Misri sijafanya kitu chochote kinachostahili nitiwe katika kifungo.”


Afazali tumwuzishe kwa hawa Waisimaeli, lakini tusiguse maisha yake, maana yeye ni ndugu yetu; yeye ni damu moja nasi.” Wandugu zake wakakubaliana naye.


Kama ukiwaelezea waziwazi wandugu maneno hayo, utakuwa mutumishi mwema wa Kristo Yesu, mwenye kukulishwa kiroho na maneno ya imani na mafundisho mazuri uliyoshika kabisa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite