Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Timoteo 1:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo, niliyeitwa kuwa mutume wa Kristo Yesu kwa amri ya Mungu Mwokozi wetu na ya Kristo Yesu tunayemutumainia.

Gade chapit la Kopi




1 Timoteo 1:1
38 Referans Kwoze  

Alifunua neno lake kwa wakati alioupanga kwa njia ya mahubiri ambayo yeye Mungu Mwokozi wetu aliyoniamuru kutangaza.


Kwa maana Mungu alitaka kuwafunulia watu hao siri ya mupango wake wenye utajiri mukubwa alioufanya kwa ajili ya mataifa yote. Nayo siri ile ni kwamba Kristo ni ndani yenu, naye ndiye anayetuletea tumaini kwamba tutashiriki katika utukufu wa Mungu.


Lakini Bwana akamwambia: “Kwenda tu, kwa maana nimemuchagua mutu huyu kwa kunitumikia, kusudi atangaze jina langu kwa mataifa, kwa wafalme na kwa Waisraeli.


yeye anayekuwa Mungu peke yake, Mwokozi wetu, asifiwe na kuwa na ukubwa, uwezo na mamlaka, kwa njia ya Yesu Kristo Bwana wetu, tangia zamani za kale, sasa na hata milele! Amina.


Tumusifu Mungu, Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo! Kwa huruma yake kubwa ametupatia uzima mupya kwa njia ya kumufufua Yesu Kristo. Na kwa hiyo tumepata tumaini lenye uzima,


Ninamushukuru Bwana wetu Kristo Yesu aliyenitia nguvu, kwa sababu alinihesabu kuwa mwaminifu hata akaniweka kwa kazi yake.


Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo na kwa wandugu wote wanaokuwa pamoja nami. Ni mimi niliyeitwa kuwa mutume, si kwa kuchaguliwa na watu, wala kwa njia ya mutu, lakini kwa njia ya Yesu Kristo na ya Mungu Baba aliyemufufua. Tunawaandikia ninyi makanisa ya Galatia.


Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo na kwa ndugu yetu Timoteo. Mimi ambaye kwa mapenzi ya Mungu, niliitwa kuwa mutume wa Kristo Yesu. Tunawaandikia kanisa la Mungu linalokuwa Korinto na watu wake wote wanaokuwa katika jimbo lote la Akaya.


Barua hii inatoka kwangu mimi Simoni Petro, mutumishi na mutume wa Yesu Kristo. Ninawaandikia ninyi mulioshiriki pamoja nasi katika imani ile inayokuwa kubwa kwa njia ya haki ya Mungu wetu na Mwokozi Yesu Kristo.


Ni kwa hiyo nimewekwa kuwa mujumbe na mutume kwa kuwafundisha watu wa mataifa mengine kusudi wapate kumwamini Mungu na kutambua ukweli. Mimi ninasema ukweli wala si uongo.


Bwana wetu Yesu Kristo mwenyewe na Mungu Baba yetu, aliyetupenda na kwa neema yake akatufariji kwa milele na kutupatia tumaini njema,


Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo na kwa ndugu yetu Sositeni. Ni mimi niliyeitwa na Mungu kwa mapenzi yake kuwa mutume wa Kristo Yesu.


Na sisi tumeona na kushuhudia kwamba Baba amemutuma Mwana wake kuwa Mwokozi wa dunia.


Kwa njia ya Kristo, ninyi munamwamini Mungu aliyemufufua na kumupa utukufu. Na kutokana na hiyo munamwamini Mungu na kumuwekea tumaini lenu.


Kwa maana Mungu amemimia Roho Mutakatifu kwa uwingi juu yetu kwa njia ya Yesu Kristo Mwokozi wetu.


Lakini wakati Mungu Mwokozi wetu alipoonyesha wema wake na upendo wake kwa watu,


Na hivi tutaishi tukingojea ule uheri tunaoutumainia, wakati utukufu wa Mungu wetu Mukubwa na Mwokozi wetu Yesu Kristo utakapotokea.


na kuiba vitu vyao. Lakini wajionyeshe kila mara kuwa waaminifu kamili, kusudi wapate kuheshimisha mafundisho juu ya Mungu Mwokozi wetu katika mambo yote.


Na ni kwa hiyo tunasumbuka na kupigana, kwa maana tunamutumainia Mungu Mwenye Uzima, Mwokozi wa watu wote na hasa zaidi Mwokozi wa waamini.


Nalo jambo hilo ni zuri na lenye kupendeza Mungu Mwokozi wetu,


Wandugu zangu, ninawajulisha kwamba Habari Njema ninayohubiri haikutungwa na mutu.


Mutangaze na kusema habari zenu. Mufanye shauri pamoja! Ni nani aliyetangaza zamani matukio ya sasa? Ni nani aliyesema mambo haya zamani? Haikukuwa mimi Yawe? Hakuna Mungu mwingine isipokuwa mimi! Mimi ni Mungu wa haki na mwokozi; hakuna mwingine isipokuwa mimi.


Kweli wewe ni Mungu mwenye kufichama, Mungu wa Israeli, Mungu mwokozi.


Ingekuwa nimechagua kazi hii kwa mapenzi yangu mwenyewe, ningeweza kungojea kupokea mushahara. Lakini kwa kuwa ni muzigo niliopewa, inanipasa kuitimiza.


Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo, mutumishi wa Kristo Yesu, niliyeitwa na Mungu kuwa mutume na niliyewekwa kwa kazi ya kutangaza Habari Njema yake.


roho yangu inamufurahia Mungu, Mwokozi wangu;


Yawe anasema: Lakini mimi ni Yawe, Mungu wenu, niliyewatoa katika inchi ya Misri; hakuna mungu mwingine lakini mimi, wala hakuna anayeweza kuwaokoa.


Maana alisema juu yao: Hakika, hawa ni watu wangu; watoto wangu ambao hawatanidanganya. Basi yeye akakuwa Mwokozi wao.


Utaletewa chakula na watu wa mataifa; wafalme watakupatia chakula bora. Hapo utatambua kwamba mimi Yawe ni Mwokozi wako; mimi Mwenye Nguvu wa Yakobo ni Mukombozi wako.


Nitawasukuma watesaji wako wakule miili yao wenyewe; watalewa damu yao wenyewe kama divai. Halafu wanadamu wote watatambua kwamba mimi ni Yawe, Mwokozi wako, Mukombozi wako, Mwenye Nguvu wa Yakobo.


Mimi peke yangu ndiye Yawe, hakuna mukombozi mwingine isipokuwa mimi.


Maana mimi ni Yawe, Mungu wenu, Mungu Mutakatifu wa Israeli, Mwokozi wenu. Ninaitoa inchi ya Misri kwa ajili ya ukombozi wenu, ninaitoa Kushi na Seba kusudi muachwe huru.


Mungu ndiye mwenye kuniokoa, nitamutegemea yeye, wala sitaogopa; Yawe ananijalia nguvu; yeye mwenyewe ndiye anayeniokoa.


Walimusahau Mungu aliyewaokoa, aliyetenda mambo makubwa katika inchi ya Misri,


Leo hii Mwokozi amezaliwa kwa ajili yenu katika muji wa Daudi, yeye ndiye Kristo na Bwana.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite