Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Samweli 8:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 Wakati huo, ninyi mutalalamika kwa sababu ya mufalme wenu ambaye mumejichagulia ninyi wenyewe. Lakini Yawe hatawajibu.”

Gade chapit la Kopi




1 Samweli 8:18
13 Referans Kwoze  

Wakati unakuja ambapo mutamulilia Yawe, lakini yeye hatawajibu. Atauficha uso wake wakati huo, kwa sababu mumetenda mambo maovu.


Munapoinua mikono yenu kwa kuomba, nitauficha uso wangu nisiwaone. Hata mukiomba sana sitawasikia, maana mikono yenu imejaa damu.


Watu watatangatanga katika inchi, wenye kufazaika sana na wenye njaa. Na wakiwa na njaa, watakasirika na kumulaani mufalme wao vilevile na Mungu wao. Wataangalia juu mbinguni


“Mwenye nyumba atakapokwisha kusimama na kufunga mulango, ninyi mutabaki inje na kuanza kupiga hodi na kusema: ‘Bwana, utufungulie.’ Naye atawajibu: ‘Sijui munatokea wapi.’


Anayekataa kusikia kilio cha masikini hatasikilizwa atakapolilia musaada.


Uliwakimbiza waadui zangu, na wale walionichukia niliwaangamiza.


Wakati atakapopatwa na taabu, Mungu atasikia kilio chake?


Atatwaa sehemu ya kumi ya kondoo wenu. Na ninyi wenyewe mutakuwa watumwa wake.


Muzigo wa baba yangu ulikuwa muzito, lakini wangu utakuwa muzito zaidi. Baba yangu aliwapiga kwa mijeledi, lakini mimi nitawapiga kwa mijeledi yenye miiba.’ ”


Asiyemwogopa Mungu ana tumaini gani wakati Mungu anapokata pumzi yake, anapomwondolea uzima wake?


Musifikiri kwamba mukono wa Mungu ni mufupi, hata asiweze kuwaokoa, au kwamba masikio yake yamefungana, hata asiweze kuwasikiliza ninyi.


Kwa sababu ya mambo hayo watasikia uzito wa kasirani yangu. Sitamwacha hata mutu mumoja aponyoke wala sitamwonea huruma mutu yeyote. Hata wakinililia kwa sauti kubwa mimi sitawasikiliza.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite