Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Samweli 7:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Samweli akawaambia Waisraeli: “Kama munamurudilia Yawe kwa moyo wenu wote, basi mutupilie mbali miungu ya kigeni na sanamu za Astaroti. Muelekeze mioyo yenu kwa Yawe, na kumutumikia yeye peke yake; naye atawaokoa kutoka katika mikono ya Wafilistini.”

Gade chapit la Kopi




1 Samweli 7:3
40 Referans Kwoze  

Lakini Yesu akamujibu: “Imeandikwa katika Maandiko Matakatifu: ‘Umwabudu Bwana Mungu wako na umutumikie yeye peke yake.’ ”


musisikilize maneno ya nabii huyo au mutabiri wa kutumia ndoto, kwa maana Yawe, Mungu wenu, anawatumia kwa kuwajaribu kusudi ajue kama munamupenda yeye Yawe, Mungu wenu, kwa moyo wenu wote na roho yenu yote.


Lakini Yesu akamwambia: “Toka wewe, Shetani! Kwa maana imeandikwa: ‘Umwabudu Bwana Mungu wako na umutumikie yeye peke yake.’ ”


Mutamwogopa Yawe, Mungu wenu, mutamutumikia yeye peke yake na kuapa katika jina lake peke yake.


Waovu waache njia zao mbaya, watu wabaya waachane na mawazo yao mabaya; wamurudilie Yawe apate kuwahurumia, wamwendee Mungu wetu maana atawasamehe.


“Sasa, basi, mumutii Yawe na kumutumikia kwa moyo wa haki na uaminifu. Muache kabisa miungu ile ambayo wazee wenu waliiabudu ngambo ya muto Furati na katika inchi ya Misri. Mumutumikie Yawe.


Naye akawaambia: “Basi, muondoe miungu ya kigeni munayokuwa nayo, mumufuate Yawe, Mungu wa Israeli, kwa moyo wenu wote.”


Mungu ni roho, nao wanaomwabudu wanapaswa kumwabudu katika roho na ukweli.”


Mumwogope Yawe, Mungu wenu, mumutumikie, muambatane naye na kuapa kwa jina lake.


vilevile wakati ule watakapokuwa katika inchi ya waadui zao, wakikugeukia kwa moyo wao wote na kwa roho yao yote, na kama wakikuomba wakielekea inchi yao ambayo uliwapatia babu zao, wakielekea muji huu ambao uliuchagua na nyumba hii ambayo nimeijenga kwa ajili ya jina lako,


“Hakuna mutu anayeweza kuwatumikia wabwana wawili. Kwa maana atamuchukia mumoja na kumupenda mwingine; au atashikamana na mumoja na kumuzarau mwingine. Hamuwezi kutumikia Mungu na kutumikia mali vilevile.


‘Watu hawa wananiheshimu kwa midomo yao. Lakini mioyo yao ni mbali nami.


Waisraeli wakatenda tena uovu mbele ya Yawe, wakatumikia Mabali, Mastaroti, na miungu ya Aramu, ya Sidona, ya Moabu, ya Amoni na ya Wafilistini. Wakamwacha Yawe wala hawakumwabudu tena.


Sasa, mumutumikie Yawe, Mungu wenu, kwa nia na moyo wote. Basi mujitayarishe kumujengea Yawe pahali patakatifu kusudi Sanduku la Agano la Yawe pamoja na vyombo vyote vitakatifu vinavyotumiwa katika ibada, viwekwe ndani ya nyumba iliyojengwa kwa ajili ya Yawe.”


Basi, Yakobo akawaambia jamaa yake na wote aliokuwa nao: “Mutupilie mbali sanamu za miungu ya kigeni munazokuwa nazo, mujitakase na kubadilisha nguo zenu.


Mutupilie mbali zambi mulizonitendea; mujipatie moyo na roho mupya. Enyi Waisraeli, mutakufa kwa sababu gani?


“Nawe Solomono mwana wangu, umujue Mungu wa baba yako, na umutumikie kwa moyo wako wote na kwa nia nzuri; yeye Yawe anachunguza mioyo na anafahamu mipango na mafikiri ya mwanadamu. Ukimutafuta yeye, utamwona; lakini ukimwacha, atakutupilia mbali milele.


Mwanadamu anapanga mipango yake, lakini neno la mwisho ni la Yawe.


Lakini, kuna wema fulani ndani yako. Umekwisha kuondoa sanamu zote za Ashera, mungu wa kike, na umejikaza sana kumutafuta Mungu kwa moyo wote.”


Kisha wakaitupilia mbali miungu ya kigeni, wakamutumikia tena Yawe. Yawe hakuweza kuvumilia zaidi kuona taabu za Waisraeli.


Watu wa Samaria wataazibiwa kwa ajili ya kosa lao; wamemwasi Mungu wao. Watauawa kwa upanga, watoto wao watapondwapondwa, na wamama wenye mimba watapasuliwa tumbo.


atakayekuomba kwa moyo wake wote wewe Yawe, Mungu wa babu zake, hata ingawa yule mutu si musafi kulingana na sheria za utakaso.”


Walimwacha Yawe, wakatumikia Mabali na Mastaroti.


Zile silaha zake waliziweka katika nyumba ya Astaroti. Kisha wakautundika mwili wake kwenye ukuta wa muji wa Betisani.


nusu ya Gileadi, Astaroti, Edirei, ambayo ilikuwa ya mufalme Ogi wa Basani. Nusu ya wazao wa Makiri mwana wa Manase, eneo hili walipewa kulingana na ukoo zao.


Nitafanya hivyo kwa sababu Solomono ameniacha, akaabudu miungu ya kigeni: Astaroti mungu wa Wasidoni, Kemosi mungu wa Wamoabu, na Milkomu mungu wa Waamoni. Solomono ameniasi, ametenda maovu mbele yangu. Hakutii masharti yangu na maagizo yangu kama Daudi baba yake alivyofanya.


Nitawapa moyo wa kujua kwamba mimi ndimi Yawe. Watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao; maana watanirudilia kwa moyo wao wote.


Labda watu wa Yuda watasikia juu ya hasara zote ambazo nimekusudia kuwatendea, kusudi kila mumoja wao auache mwenendo wake mubaya, nami nipate kuwasamehe makosa yao na zambi yao.


Basi, uwaambie Waisraeli kwamba: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Munirudilie, na kuacha kuziabudu sanamu zenu za miungu. Muache kufanya machukizo.


Kisha kutoka humohumo katika inchi mutamutafuta Yawe, Mungu wenu, nanyi mutamupata kama mukimutafuta kwa moyo wote na roho yote.


Basi, Waisraeli walitenda uovu mbele ya Yawe na kuabudu Mabali.


mutaniabudu mimi Yawe, Mungu wenu, nami nitawaokoa kutoka katika mikono ya waadui zenu.”


Zaidi ya hayo aliharibu kule Beteli pahali pa kuabudia palipojengwa na mufalme Yeroboamu mwana wa Nebati ambaye aliwasukuma watu wa Israeli watende zambi. Aliharibu mazabahu hayo na kuvunja mawe yake vipandevipande, na kisha akaviponda mpaka vikakuwa mavumbi. Vilevile akachoma sanamu ya Ashera.


Lakini hakuharibu pahali pa kutambikia sadaka juu ya kilima. Watu walikuwa wangali hawajamugeukia na kumwabudu Mungu wa babu zao kwa mioyo yao.


Yawe anasema hivi: Ukitaka kurudi, ee Israeli, unirudilie mimi. –Ni ujumbe wa Yawe.– Ukiviondoa vitu vyako vya kuchukiza mbele yangu, usipotangatanga huko na huko,


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite