Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Samweli 7:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Miji yote ya Waisraeli ambayo Wafilistini waliiteka kati ya Ekuroni na Gati ilirudishiwa kwa Waisraeli. Waisraeli walikomboa inchi yao kutoka kwa Wafilistini. Tena kulikuwa amani kati ya Waisraeli na Waamori.

Gade chapit la Kopi




1 Samweli 7:14
8 Referans Kwoze  

Hawakuwaua watu wa mataifa kama vile Yawe alivyowaamuru.


Lakini Sisera akakimbia kwa miguu mpaka katika hema ya Yaeli, muke wa Heberi Mukeni. Alifanya hivyo kwa sababu kulikuwa amani kati ya mufalme Asikie wa Hazori na jamaa ya Heberi.


Muangamize taifa lolote ambalo Yawe, Mungu wenu atalitia katika mikono yenu, wala musilionee huruma. Musiabudu miungu yao, maana jambo hili litakuwa mutego kwenu.


Vilevile, kisha Yawe, Mungu wenu, kuyatia katika mikono yenu, mutayashinda na kuyaangamiza kabisa. Musifanye agano lolote nayo wala musiyahurumie.


Waamaleki wanakaa katika eneo la Negebu; Wahiti, Wayebusi na Waamori wanakaa katika eneo la milima, na Wakanana wanakaa karibu na bahari ya Mediteranea na karibu na kingo za muto Yordani.


Kisha wafalme hao watano wa Waamori: mufalme wa Yerusalema, mufalme wa Hebroni, mufalme wa Yarmuti, mufalme wa Lakisi na mufalme wa Eguloni, wakaunganisha waaskari wao, wakaenda nao mpaka Gibeoni. Wakapiga kambi kuuzunguka muji huo, wakaushambulia.


Kisha ukaendelea upande wa kaskazini wa Ekuroni, ukazunguka kuelekea Sikeroni ambapo ulipita karibu na mulima Bala mpaka Yabuneli ukaishia katika bahari ya Mediteranea.


Nyuma ya hayo, mufalme Daudi aliwashinda na kuwanyenyekeza Wafilistini. Akakamata muji wa Gati pamoja na vijiji vyake vilivyokuwa vya Wafilistini.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite