Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Samweli 6:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Wale ngombe walikwenda moja kwa moja kuelekea muji wa Beti-Semesi bila kupinda kushoto au kuume, walikuwa wanalia walipokuwa wanakwenda. Wale wafalme watano wa Wafilistini waliwafuata mpaka kwenye mupaka wa Beti-Semesi.

Gade chapit la Kopi




1 Samweli 6:12
7 Referans Kwoze  

Waisraeli wakamwambia: Sisi tutafuata njia kubwa; kama sisi na mifugo yetu tukikunywa maji yenu, tutalipa. Tunachoomba tafazali uturuhusu tu, tupite kwa miguu wala hatutaki neno lolote lingine.


Lakini muangalie. Ikiwa gari hilo linakwenda moja kwa moja kuelekea inchi yake, ni kusema kwenye muji wa Beti-Semesi, basi, pale tutajua kwamba aliyetuletea pigo hili ni Mungu wa Israeli. Lakini kama haliendi kule, basi, tutajua kwamba sio mukono wake uliotupiga, lakini hasara hii imetupata kwa bahati mbaya.”


Lile Sanduku la Yawe wakalitia kwenye gari hilo pamoja na kile kibweta chenye kuwa na sanamu za zahabu za panya na zile za majipu.


Watu wa Beti-Semesi walikuwa wanavuna ngano katika bonde. Walipoangalia juu na kuliona Sanduku la Yawe, wakafurahi sana.


Wale wachawi wakamwambia mufalme wa Misri: “Hii ni kazi ya mukono wa Mungu.” Lakini moyo wa mufalme ukaendelea kuwa mugumu, wala hakuwasikiliza Musa na Haruni. Ikakuwa kama vile Yawe alivyokuwa amesema.


ambako ulipinda upande wa magaribi kuelekea Seiri; ukapita kaskazini ya mulima wa Yerimu, ni kusema Kesaloni, na kuteremuka mpaka Beti-Semesi ambapo ulipita karibu na Timuna.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite