Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Samweli 4:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Waaskari walioponyoka walipofika kwenye kambi, wazee wa Israeli walisema: “Kwa nini Yawe amewaacha Wafilistini watushinde leo? Tuende tulilete Sanduku la Agano la Yawe kutoka Shilo, kusudi aweze kwenda nasi katika vita na kutuokoa kutoka waadui zetu.”

Gade chapit la Kopi




1 Samweli 4:3
34 Referans Kwoze  

Ijapokuwa mumekwisha kujua kabisa mambo haya yote, ninataka kuwakumbusha namna Bwana alivyowaokoa Waisraeli kutoka katika inchi ya Misri, lakini kisha, akawaangamiza wale waliokataa kuamini.


Maji haya ni mufano wa ubatizo unaowaokoa ninyi sasa. Ubatizo ule si kwa ajili ya kusafisha uchafu wa mwili lakini ni njia ya kufanya mapatano na Mungu katika zamiri safi. Nao unawaokoa ninyi kwa njia ya ufufuko wa Yesu Kristo,


Ndani ya chumba kile kulikuwa chombo cha kufukizia ubani, kilichotengenezwa na zahabu. Na kulikuwa vilevile Sanduku la Agano lililopakaliwa zahabu pande zote. Ndani ya sanduku lile kulikuwa kopo la zahabu lenye mana, na fimbo ya Haruni iliyoota vichipukizi juu yake. Kulikuwa vilevile vibao vya mawe vyenye Maandiko ya Agano la Mungu.


Kwa inje watajionyesha kama watu wenye kushikamana na ibada, lakini wanazarau uwezo wake. Ujiepushe na watu hao.


Musitumainie maneno haya ya udanganyifu mukisema: Hili ni hekalu la Yawe, hekalu la Yawe, hakika hili ni hekalu la Yawe.


Siku hizo, wakati mutakapokuwa mumeongezeka na kuwa wengi katika inchi, watu hawatalitajataja tena Sanduku langu la Agano. –Ni ujumbe wa Yawe.– Hawatalifikiri juu yake kabisa, wala hawatalikumbuka tena; hawatalihitaji, wala hawatatengeneza lingine.


Ninyi munaniuliza: Kwa nini tunafunga kula lakini wewe hauoni? Mbona tunajitesa, lakini wewe haujali? Ukweli ni kwamba wakati munapofunga kula, munatafuta tu furaha yenu wenyewe na kuwagandamiza watumishi wenu!


Yawe anasema hivi: Kama nimeachana na mama yako Yerusalema, barua ya kuachana iko wapi? Nilikuwa na deni ya nani kwa kuwauzisha? Mukumbuke kwamba muliuzishwa kwa ajili ya maovu yenu, mama yenu alifukuzwa kwa ajili ya makosa yenu.


Mbona umeficha mukono wako wa kuume? Kwa nini haunyooshi mukono na kuwapiga?


Mashairi ya Asafu. Kwa nini, ee Mungu, umetutupilia kabisa? Mbona hasira yako inawaka juu ya kondoo wako?


Wakati mufalme Daudi alipokuwa akiikaa katika nyumba yake ya kifalme, siku moja akamwita nabii Natani, na kumwambia: “Angalia, mimi ninakaa katika nyumba nzuri iliyojengwa na miti ya mwerezi, lakini Sanduku la Agano la Yawe linakaa ndani ya hema.”


Kisha mufalme akamwambia Zadoki: “Urudishe Sanduku la Agano la Mungu katika muji. Kama nimepata kukubaliwa mbele ya Yawe, bila shaka atanirudisha na kunijalia kuliona tena Sanduku lake na kuyaona makao yake.


Saulo akamwambia kuhani Ahiya: “Ulete hapa Sanduku la Agano la Mungu.” (Wakati huo Sanduku la Agano la Mungu lilikuwa pamoja na Waisraeli.)


Yoshua akasema: “Ole wetu, ee Bwana wetu Yawe! Kwa nini umetuvukisha muto Yordani kwa kututia katika mikono ya Waamori kusudi watuangamize? Tungalifurahi kubaki ngambo ya muto Yordani!


Ninyi mutawaambia: ‘Sanduku la Agano la Yawe lilipopitishwa katika muto Yordani, maji ya muto huo yalizuiliwa yasitiririke!’ Kwa hiyo mawe haya yatakuwa ukumbusho kwa Waisraeli milele.”


“Mutwae kitabu hiki cha sheria, mukiweke karibu na Sanduku la Agano la Yawe, Mungu wenu, kusudi kikuwe ushuhuda juu yenu.


Na jibu hili litatolewa: ‘Ni kwa sababu walivunja agano la Yawe, Mungu wa wazee wao ambalo alifanya nao alipowatoa katika inchi ya Misri.


Musa akawapeleka kwa vita chini ya uongozi wa Finehasi mwana wa kuhani Eleazari, akiwa na vyombo vya Pahali Patakatifu na baragumu za kutoa kitambulisho.


Kila wakati sanduku liliposafiri kwenda mbele, Musa alisema: Inuka, ee Yawe, uwatawanye waadui zako, na hao wanaokuchukia uwafanye wakimbie kutoka mbele yako.


Basi, watu wakasafiri toka Sinai, mulima wa Yawe, mwendo wa siku tatu. Sanduku la Agano la Yawe liliwatangulia mwendo wa siku tatu, kwa kuwatafutia pahali pa kupigia kambi.


Basi, Yoshua mwana wa Nuni, akawaita makuhani, akawaambia: “Mulibebe Sanduku la Agano na makuhani saba watwae mabaragumu saba ya kondoo dume, watangulie mbele ya Sanduku la Yawe.”


Ee Bwana, niseme nini wakati Waisraeli wamewakimbia waadui zao?


Alipomwachisha kunyonya alimupeleka pamoja na ngombe dume wa miaka mitatu, gunia la unga na karabia ya divai. Hana alimwingiza mutoto kwenye nyumba ya Yawe kule Shilo, naye mutoto alikuwa mudogo tu.


Wafilistini waliwashambulia Waisraeli, na nyuma ya mapigano makali, Waisraeli walishindwa. Waisraeli elfu ine waliuawa kwenye uwanja wa vita.


Musifikiri kwamba mukono wa Mungu ni mufupi, hata asiweze kuwaokoa, au kwamba masikio yake yamefungana, hata asiweze kuwasikiliza ninyi.


Zambi zenu ndizo zinazowatenga na Mungu wenu, zambi zenu zimemufanya ajifiche mbali nanyi hata asiweze kuwasikiliza ninyi.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite